11.3 Kusikiza mpigo wa moyo wa mtoto

Mpigo wa moyo wa mtoto hukufahamisha kuhusu mlalo wa mtoto ndani ya mama na kuhusu afya ya mtoto. Sikiza mpigo wa moyo katika kila safari yake ya utunzaji katika ujauzito kuanzia miezi mitano. Mara nyingi madaktari na wakunga hurejelea mpigo wa moyo.

Kufikia miezi miwili ya mwisho ya ujauzito, unaweza kusikia mpigo wa moyo wa fetasi mara nyingi ukiwa katika chumba kisicho na kelele kwa kuweka sikio lako kwenye fumbatio la mama (Mchoro 11.10a). Ni rahisi kusikia mpigo wa moyo kwa stethoskopu (Mchoro 11.10b) au fetoskopu (Mchoro 11.10c na d). Iwapo huna fetoskopu, unaweza kujitengenezea moja kutoka kwa mbao, mchanga au mwanzi.

Mchoro 11.10 Kusikiza mpigo wa moyo wa fetasi kwa (a) sikio lako kwenye fumbatio la mama, au (b) kwa stethoskopu, au (c) na (d) kwa fetoskopu.

Mpigo wa moyo wa fetasi ni tulivu na wa haraka. Unaweza kusikika kama mpigo mwepesi wa saa chini ya mto, ingawa kwa kasi. Mpigo wa moyo wa fetasi ni takriban mara mbili zaidi ukilinganishwa na wa moyo wa mtu mzima - kwa kawaida mipigo 120 hadi 160 kwa dakika. Hamna haja ya kuhesabu mipigo ya moyo hadi mwanamke atakapoanza leba. Kusikia mpigo dhahiri wa moyo wa fetasi wakati wa safari ya utunzaji katika ujauzito hudhibitisha kuwa mtoto yuko hai.

Ukisikia sauti ya mtindo fulani (shee-oo, shee-oo, shee-oo), huenda unasikia mpwito wa ateri wa mtoto kwenye kiungamwana. Sauti kwenye kiungamwana hukuonyesha jinsi moyo wa mtoto unavyopiga haraka, bali hazikusaidii kujua mkao wa mtoto kwenye uterasi.

Mpigo wa moyo ukiwa polepole, huenda unasikia mpwito wa ateri wa mama badala ya ule wa mtoto. Jaribu kusikiza kwenye sehemu tofauti kwa fumbatio lake.

11.2.5 Kumwuliza mama kuhusu kucheza kwa mtoto

11.3.1 Kujua mkao wa mtoto kwenye uterasi kwa kusikiza mpigo wa moyo