11.4 Cha kufanya ukipata dalili za hatari

11.4.1 Mtoto ametanguliza matako

Watoto waliotanguliza matako mara nyingi huzaliwa bila matatizo yoyote, hasa ikiwa mama amewahi kuzaa watoto wengine na alizaa kwa urahisi. Lakini watoto waliotanguliza matako wana uwezekano mkubwa wa kukwama, au kuwa na matatizo mengine hatari.

Iwapo mtoto ametanguliza matako kufikia juma la 36 (miezi 8), mpe mwanamke huyo rufaa aende katika kituo cha afya. Usijaribu kumgeuza mtoto aliyetanguliza matako (tazama Kisanduku 11.1).

Kisanduku 11.1 Usijaribu kumgeuza mtoto aliyetanguliza matako!

Ni mkunga, afisa wa afya au daktari aliyefunzwa kugeuza mtoto aliyetanguliza matako anayepaswa kujaribu kufanya hivyo na inapaswa kufanyika hospitalini. Kujaribu kugeuza mtoto kwa kufinya uterasi ni hatari sana. Hata mkunga, afisa wa afya au daktari asijaribu kumgeuza mtoto ikiwa kiowevu cha amnioni cha mama hakijatoka, au ikiwa ametokwa na damu ukeni, amekuwa na shinikizo la juu la damu, upasuaji kwenye uterasi yake, au upasuaji wa kuzaa.

Iwapo mtoto hayuko katika hali ya kichwa chini leba inapoanza, ni salama zaidi kwa mama kuzalia hospitalini. Mkunga, afisa wa afya au daktari anaweza kutumia fosepu (vifaa vya kuvuta) mtoto akikwama. Au wanaweza kufanya upasuaji wa kuzaa.

11.3.1 Kujua mkao wa mtoto kwenye uterasi kwa kusikiza mpigo wa moyo

11.4.2 Mtoto amelala kingamo