12.1.1 Kichefuchefu, kutapika, na hiparemesisi gravidaramu

Wanawake wengi hupata kichefuchefu na kutapika katika trimesta ya kwanza (miezi 3) ya ujauzito ambayo mara nyingi huitwa kigegezi cha asubuhi. Hutokea sana asubuhi mwanamke anapotoka kitandani. Utoaji mate kupindukia ni tatizo lisilotokea sana bali linalokera mno na linalohusiana na hali iitwayo hiparemesisi gravidaramu – inayosababishwa na kichefuchefu kikali cha mara kwa mara na kutapika kupindukia katika ujauzito.

Hiparemesisi humaanisha ‘kutapika kupindukia’. Gravidaramu humaanisha ‘katika ujauzito’.

Hiparemesisi gravidaramu ni tatizo kali kiasi kwamba mwanamke aliye nalo anapaswa kulazwa hospitalini au katika kituo cha afya.

Utambuzi wa hiparemesisi gravidaramu hufanywa mwanamke akipoteza kilo 5 au zaidi za uzani wa mwili wake kutokana na kutapika mara kwa mara, kupoteza viowevu vya mwili na kichefuchefu, na hali hii humfanya aogope kula, na huthibitishwa kwa kuwepo kwa kemikali za asidi (ketoni) katika mkojo wake. Mwili huanza kutoa ketoni unapoanza kusaga protini kwenye misuli kutokana na ukosefu wa chanzo mbadala cha nguvu ili kumweka mtu hai. Ketoni hizo zinaweza kugunduliwa kwenye mkojo kwa kipimo cha dipstick unachoweza kumfanyia mwanamke nyumbani kwake au katika Kituo cha Afya iwapo umepewa dipstick zifaazo na kuonyeshwa jinsi ya kuchunguza na kutambua mabadiliko ya rangi iwapo ketoni zimo.Matokea chanya ya kipimo hiki humaanisha kuwa sharti apewe rufaa mara moja ili aweze kupata lishe, viowevu vya mwili na kemikali muhimu mbadala, na apate matibabu ya kumkinga ili asije akakumbwa na matatizo haya tena.

Udhibiti wa kichefuchefu kisicho kikali

Ikiwa kichefuchefu si kikali, mhimize mwanamke kujaribu moja ya tatuzi hizi:

  • Kabla ya kulala au usiku, kula chakula kilicho na protini, kama vile maharagwe, njugu au jibini.
  • Kula ndizi chache, mkate mkavu, kita kavu, au vyakula vingine vya mbegu anapoamka asubuhi.
  • Kula milo mingi midogo badala ya milo miwili au mitatu mikubwa, na kunywa kiasi kidogo cha viowevu mara kwa mara.
  • Kunywa kikombe cha mnanaa, mdalasini au chai ya tangawizi mara mbili au tatu kwa siku kabla ya kula. Weka kijiko kimoja cha chai cha mnanaa, au kijiti cha mdalasani kwenye kikombe cha maji moto kisha ungoje kwa dakika chache kabla ya kunywa. Kutengeneza chai ya tangawizi, chemsha mzizi wa tangawizi uliokatwa vipande au kupondwa kwa angalau dakika 15.

12.1 Matatizo yanayohusiana na mmeng’enyo wa chakula na chakula

12.1.2 Kutopenda chakula na tamaa ya chakula