12.1.2 Kutopenda chakula na tamaa ya chakula

Huenda mwanamke mjamzito akachukia kighafla chakula alichopenda hapo awali. Ni SAWA kutokula chakula hicho, na huenda akaanza kukipenda tena baada ya kuzaa. Anafaa kuwa makini kuhakikisha kuwa lishe yake ina vyakula vyenye virutubishi vingi. Utajifunza ushauri wa kumpa mwanamke kuhusu lishe bora katika ujauzito katika Kipindi cha 14.

Tamaa ya chakula (pia hujulikana kama pika) ni hamu kubwa ya kula aina fulani ya chakula, au hata kitu ambacho si chakula kama vile udongo mweusi, chaki au mchanga (Mchoro 12.1). Mwanamke akipata tamaa ya vyakula vyenye virutubishi (kama maharagwe, mayai, matunda au mboga), ni VYEMA kwake kula kiasi anachotaka.

Mchoro 12.1  Tamaa ya chakula ni kawaida mwanzoni mwa ujauzito.

Mwanamke aliye na tamaa ya kula vitu visivyo chakula kama vile udongo au mchanga anafaa kushauriwa asivile. Vinaweza kumsumisha yeye na mtoto wake. Pia vinaweza kumpa vimelea kama minyoo, vinavyoweza kumfanya awe mgonjwa. Badala yake mhimize ale vyakula vyenye ayoni na kalisi (tazama ushauri katika Mchoro 12.1).

12.1.1 Kichefuchefu, kutapika, na hiparemesisi gravidaramu

12.1.3  Kiungulia