12.1.3  Kiungulia

Hisia ya mchomo au maumivu tumboni au kati ya matiti, huitwa kutomeng’enyeka au kiungulia. Kiungulia hutokea kwa sababu mtoto anayekua hujaza fumbatio la mama na kusukuma tumbo juu zaidi ya kawaida (Mchoro 12.2). Asidi zilizo kwenye tumbo la mama zinazosaidia katika umeng'enyaji wa chakula husukumwa juu kwenye kifua chake ambapo husababisha hisia ya mchomo. Mhakikishie kuwa hii si hatari na huisha baada ya kuzaa.

Mchoro 12.2  Kiungulia katika ujauzito kinaweza kutokana na mtoto kujaa kwenye fumbatio la mama.

Udhibiti

Hapa kuna mambo ambayo mwanamke anaweza kufanya ili kuhisi utulivu zaidi:

  • Kutojaza tumbo yake kwa kula milo midogo midogo mara kwa mara, na kwa kula vyakula na kunywa viowevu vikiwa kando.
  • Kuepuka vyakula vyenye viungo au mafuta, kutumia kahawa, au kuvuta sigara kwa sababu hivi vyote vinaweza kusababisha mchomo tumboni.
  • Kula papaya au nanasi mara kwa mara kwa sababu matunda haya yana enzaimu (kemikali maalum) zinazosaidia tumbo kumeng'enya chakula.
  • Kuweka kichwa chake juu zaidi ya tumbo anapolala au kupumzika. Hii itasaidia kudumisha asidi za tumbo kwenye tumbo na si kifuani.
  • Kutuliza asidi tumboni kwa kunywa maziwa, au dawa za kudhibiti asidi zenye kiwango cha chini cha chumvi (kiowevu au tembe zinazotuliza tumbo) zilizo na asprin, lakini mshauri ajaribu kutumia mbinu zingine kabla ya kutumia dawa kama za kudhibiti asidi.

12.1.2 Kutopenda chakula na tamaa ya chakula

12.1.4  Uyabisi wa utumbo