12.1.4  Uyabisi wa utumbo

Wanawake wengine wajawazito huwa na ugumu wa kupitisha kinyesi. Hii huitwa uyabisi wa utumbo. Husababishwa na mabadiliko katika homoni ambayo hupunguza mienendo ya misuli ya utumbo (usukumaji wa chakula chini kwenye koromeo), inayosukuma chakula kwenye matumbo. Hii husababisha ongezeko katika ‘muda wa kuondoa’, muda wa kumeng'enywa kwa chakula na uchafu unaondolewa kama kinyesi.

Udhibiti

Kuzuia au kutibu uyabisi wa utumbo, mwanamke mjamzito anapaswa:

  • Kula matunda na mboga kwa wingi.
  • Kula nafaka nzima (wali wa rangi ya kahawia na ngano, badala ya wali au unga mweupe).
  • Kunywa angalau vikombe vinane vya maji kwa siku.
  • Kutembea na kufanya mazoezi kila siku.
  • Jaribu tiba za nyumbani au mimea ambazo zitalainisha kinyesi au kukifanya kiwe telezi, kwa mfano, tiba zinazotokana na mbegu za telba, matunda fulani, au mimea yenye nyuzi kama vile gomeni.

12.2 Vena zilizovimba