12.2.1  Uvarikosi (vena varikosi)

Uvarikosi wa viungo vya uzazi unaweza kusababisha kuvuja damu ukipasuka wakati wa kuzaa, kwa hivyo, mpe mwanamke aliye na tatizo hili rufaa aende katika kituo cha afya.

Vena zilizovimba za buluu zinazotokea kwa miguu huitwa uvarikosi, au vena varikosi, na hutokea sana katika ujauzito. Wakati mwingine, vena hizi huuma. Shinikizo kutoka kwa uterasi inayokua, kwa vena zinazorudisha damu kwenye moyo kutoka kwenye miguu ni kisababishi kikubwa cha uvarikosi kwa vena za miguu. Ni nadra sana kwa vena za jenitalia za nje kuvimba, lakini zikivimba huuma sana.

Udhibiti

Ikiwa vena zilizovimba ni za miguu, zinaweza kutulia mwanamke akiweka miguu yake juu mara kwa mara. Stoki thabiti au bendeji nyumbufu pia huweza kusaidia. Ikiwa vena zilizovimba zipo karibu na jenitalia, chupi maalum ya kushikilia au padi ya usafi inaweza kumsaidia kwa kushikilia.

12.2 Vena zilizovimba

12.2.2  Hemoroidi