12.2.2  Hemoroidi

Hemoroidi ni vena zilizovimba kwenye eneo karibu na mkundu. Zinaweza kuchoma, kuuma au kuwasha. Wakati mwingine huvuja damu mwanamke anapopitisha kinyesi, hasa ikiwa ana uyabisi wa utumbo. Kuketi au kusimama kwa muda mrefu kunaweza kuendeleza athari za hemoroidi.

Udhibiti

Mwanamke anafaa kujaribu kuepuka uyabisi wa utumbo kwa kula matunda, mboga kwa wingi na kunywa maji mengi. Kulazimisha kupitisha kinyesi huendeleza athari za hemoroidi. Kuketi kwenye maji baridi au kulala chini husaidia.

12.2.1  Uvarikosi (vena varikosi)

12.3  Maumivu