12.3  Maumivu

12.3.1  Maumivu ya mgongo

Wanawake wengi wajawazito hukumbwa na maumivu ya mgongo. Uzani wa mtoto, uterasi na kiowevu cha amnioni hubadili mkao wake na kuweka mkazo kwenye mifupa na misuli ya mwanamke huyo. Kusimama mahali pamoja kwa muda mrefu, kuinama au kazi nyingi za sulubu, zinaweza kusababisha maumivu ya mgongo. Aina nyingi za maumivu ya mgongo ni kawaida katika ujauzito lakini pia zinaweza kusababishwa na maambukizi ya figo.

Udhibiti

Mhimize mume, watoto, jamaa wengine au marafiki wa mwanamke huyu kuusinga mgongo wake. Kitambaa chenye joto au chupa yenye maji moto kwenye mgongo wake pia vinaweza kumtuliza. Pia jamaa zake wanaweza kusaidia kwa kufanya baadhi ya kazi nzito kama vile kubeba watoto wadogo, kufua, kulima, na kusaga nafaka. Chupi inayokaza, au mshipi unaovaliwa kwenye nyonga, pamoja na kupumzika kitandani mara kwa mara kunaweza kupunguza maumivu ya mgongo.

12.3.2  Maumivu ya viungo