12.3.2  Maumivu ya viungo

Homoni katika trimesta ya tatu (miezi sita hadi tisa ya ujauzito) huzichochea viungo vya mwanamke na kuzifanya kuwa laini na legevu. Hii hufanya jointi zake ziweze kupindika, zikiwemo jointi kati ya mifupa kwenye pelvisi yake (kumbuka anatomia ya pelvisi katika Kipindi cha 6, hasa Mchoro 6.1).

  • Je, unafikiri ni kwa nini kulegea huku kwa viungo vya pelvisi ni muhimu katika kipindi cha mwisho cha ujauzito?

  • Husaidia kutengeza nafasi inayoweza kupanuka kwenye pelvisi ili mtoto aweze kupita kwenye njia ya uzazi katika leba na kuzaa.

    Mwisho wa jibu

Wakati mwingine, viungo vya mwanamke mjamzito hulegea sana na kuwa zenye kutatiza, hasa nyonga, na huenda akapoteza uthabiti wa pelvisi yake, jambo linalosababisha maumivu. Maumivu ya viungo si hatari, lakini mwanamke anaweza kuteguka kwenye vifundo vya miguu au viungo vingine.

12.3.3  Kukakamaa kwa miguu