12.3.6  Maumivu ya kichwa na kipandauso

Maumivu ya kichwa hutokea sana katika ujauzito bali si hatari. Maumivu haya ya kichwa yanaweza kuisha mwanamke akipumzika na kutulia zaidi, akinywa juisi au maji zaidi, au akisinga paji la uso kwa upole. Ni SAWA kwa mwanamke mjamzito kunywa tembe mbili za paracetamol na glasi ya maji mara moja baada ya muda fulani. Hata hivyo, maumivu ya kichwa mwishoni mwa ujauzito yanaweza kuwa ishara ya hatari ya priklampsia, hasa ikiwa pia kuna shinikizo la juu la damu, au kuvimba kwa uso au mikono. Priklampsia imejadiliwa kwa kina baadaye katika moduli hii, katika Kipindi cha 19.

Ukishuku kuwa kuna priklampsia, mpe mwanamke rufaa aende katika kituo cha afya kilicho karibu mara moja.

Wanawake wengine hupata maumivu ya kipandauso kichwani. Haya huwa maumivu makali ya kichwa, mara nyingi kwenye pande za kichwa. Mwanamke anaweza kuona matone na kuhisi uchefuchefu. Mwanga mkali au mwanga wa jua unaweza kuendeleza maumivu haya. Kipandauso kinaweza kuwa kibaya zaidi katika ujauzito.

Udhibiti

Kwa bahati mbaya, dawa za kipandauso ni hatari sana katika ujauzito. Zinaweza kusababisha leba kuanza kabla ya wakati, na pia zinaweza kumdhuru mtoto. Ni bora kwa mwanamke mjamzito aliye na kipandauso kunywa miligramu 500 hadi 1000 za paracetamol na glasi ya maji kisha apumzike katika chumba chenye giza. Ingawa kahawa na chai si bora katika ujauzito, ni SAWA mara kwa mara, na huenda zikasaidia katika kutibu kipandauso.

12.3.5  Mikakamao kwenye fumbatio mapema katika ujauzito

12.4 Matatizo madogo katika mifumo mingine ya mwili