12.4 Matatizo madogo katika mifumo mingine ya mwili

12.4.1  Edema

Ukishuku kuwa edema inaweza kuwa ishara ya priklampsia, mpe mwanamke huyo rufaa aende katika kituo cha afya kilicho karibu mara moja.

Kuvimba nyayo na vifundo vya miguu hutokea sana katika ujauzito, hasa alasiri au katika hali ya anga yenye joto. Kuvimba huku hutokana na edema,ambayo ni ubakizaji wa viowevu kwenye tishu za mwili. Chini ya nguvu za uzito, kiowevu kilichobakizwa huteremka mwilini na kujikusanya kwenye nyayo. Mhimize mwanamke huyo kuketi akiwa ameinua nyayo zake mara nyingi iwezekanavyo ili kuwezesha viowevu hivi kufyonzeka na kurudi katika mfumo wa mzunguko wa damu. Kuvimba kwa miguu si hatari, lakini uvimbe mkali mwanamke anapoamka asubuhi, au kuvimba kwa mikono na uso wakati wowote, kunaweza kuwa ishara za priklampsia ambayo ni hali mbaya zaidi (hata ya kuhatarisha maisha).

Udhibiti

Mwanamke anaweza kupata nafuu kutokana na uvimbe kwenye miguu akiweka miguu yake juu kwa dakika chache angalau mara mbili au tatu kwa siku, akiepuka kula vyakula tayari vilivyo na chumvi nyingi, na akinywa maji au juisi za matunda kwa wingi.

12.3.6  Maumivu ya kichwa na kipandauso

12.4.2  Ukojoaji wa mara kwa mara