12.4.3  Mchozo ukeni

Mchozo ni unyevunyevu utokao ukeni ambao kila mwanamke huwa nao. Mwili wa mwanamke hutumia mchozo huu kujisafisha kutoka ndani. Kwa wanawake wengi, mchozo huu hubadilika wakati wa hedhi. Wanawake wajawazito hupata mchozo mwingi, hasa wanapoelekea mwisho wa ujauzito. Unaweza kuwa angavu au wa manjano. Hii ni kawaida. Hata hivyo, mchozo huu unaweza kuwa ishara ya maambukizi uwapo mweupe, wa kijivu, kijani, wenye viwimbi, wenye harufu mbaya, au uke ukiwasha au ukiwa wenye kuchomeka.

Unafaa kutoa rufaa kwa kila kisa cha maambukizi ya uke kwenda katika kituo cha afya kilicho karibu.

12.4.2  Ukojoaji wa mara kwa mara

12.4.4  Kuhisi joto au kutokwa na jasho jingi