12.4.5  Disnia (upungufu wa pumzi)

Wanawake wengi hupata upungufu wa pumzi (hawawezi kupumua kama kawaida) wakiwa wajawazito. Hali hii huitwa disnia.

  • Je, kwa nini unafikiri upungufu wa pumzi ni tatizo linalotokea sana mwishoni mwa ujauzito?

  • Upungufu wa pumzi hutokana na mtoto anayekua kujaza mapafu ya mama na kumkosesha nafasi ya kutosha ya kupumua.

    Mwisho wa jibu

Udhibiti

Wahakikishie wanawake walio na upungufu wa pumzi mwishoni mwa ujauzito kuwa ni jambo la kawaida. Lakini ikiwa mwanamke ni mdhaifu na mwenye uchovu, au akipungukiwa na pumzi kila wakati, anafaa kuchunguzwa kwa ishara za ugonjwa, matatizo ya moyo, anemia, na lishe duni. Pata ushauri wa kiafya ukishuku kuwa huenda ana mojawapo ya matatizo haya.

12.4.4  Kuhisi joto au kutokwa na jasho jingi

12.4.6  Ugumu wa kuamka na kulala