12.4.6  Ugumu wa kuamka na kulala

Ni vyema mwanamke mjamzito kutolala chali, kwa sababu huenda ikawa vigumu kuamka tena, na kwa kuwa mwanamke akiwa ameulalia mgongo wake, uzito wa uterasi huifinya mishipa mikubwa ya damu ambayo hurudisha damu kwa moyo. Hii inaweza kupunguza usambazaji wa oksijeni kwa ubongo wake kwa muda na kumfanya ahisi kizunguzungu. Ikiwa mwanamke anataka kuulalia mgongo wake, anafaa kuweka kitu chini ya mgongo na chini ya magoti yake ili asilale chali kikamilifu.

Mwanamke mjamzito pia anafaa kuwa makini anavyoamka. Hastahili kuamka kama mwanamke katika Mchoro 12.3 (a). Badala yake, anafaa kugeuka upande mwingine na kujisukuma juu kwa mikono yake, jinsi ilivyo katika Mchoro 12.3 (b).

Mchoro 12.3 (a) Kuamka bila kugeuka upande mmoja kwanza kunaweza kurarua misuli ya fumbatio. (b) Kugeuka upande na kujisukuma juu kwa mikono ni salama sana na atahisi utulivu.

12.4.5  Disnia (upungufu wa pumzi)

12.4.7  Kloasma (barakoa ya ujauzito)