12.5.3  Matatizo ya usingizi

Baadhi ya wanawake wajawazito huhisi usingizi sehemu kubwa ya siku. Hii ni kawaida katika miezi mitatu ya kwanza. Miili yao huwaelekeza kupunguza shughuli na kupumzika. Hakuna haja ya kuingilia isipokuwa mwanamke akihisi udhaifu, ambao unaweza kuwa ishara ya tatizo kubwa zaidi, kama vile ugonjwa, mfadhaiko au anemia.

Wakati mwingine wanawake wajawazito huwa na matatizo ya kulala; wanaweza kuwa na ugumu wa kupata usingizi au waamke baada ya muda mfupi na wasipate usingizi tena. Tatizo hili huitwa insomnia (ukosefu wa usingizi).

Udhibiti wa insomnia

Iwapo mwanamke mjamzito hawezi kulala kwa sababu ya wasiwasi au kuhangaika, anaweza kusaidika:

  • Akilalia upande na kitu cha kustarehesha kati ya magoti yake na kwenye sehemu ya chini ya mgongo wake. Anaweza kutumia mto, blanketi iliyokunjwa, majani ya ndizi, au kitu kingine laini.
  • Mtu akimsinga.
  • Akinywa chai za mitishamba zitakazomsaidia kulala.

12.5.2  Wasiwasi na hofu

12.5.4  Ndoto za ajabu na majinamizi