Muhtasari wa Kipindi cha 12

Katika Kipindi cha 12, umejifunza kuwa:

  1. Mwili wa mwanamke hubadilika katika ujauzito. Mabadiliko haya wakati mwingine yanaweza kukosesha utulivu, lakini ni ya kawaida na huisha baada ya mtoto kuzaliwa.
  2. Unaweza kupunguza mengi ya matatizo madogo katika ujauzito kwa kupata ushauri kuhusu lishe, mazoezi, na kwa tiba rahisi za nyumbani zinazoaminika kuwa salama na huwasaidia wanawake kuhisi vyema.
  3. Wakati mwingine matatizo haya madogo yanaweza kuwa mabaya, au kuashiria tatizo lingine la kiafya linalohitaji rufaa kwenye kituo cha afya.
  4. Tiba zingine (kama vile dawa za kipandauso) ni hatari kwa wanawake wajawazito na zinaweza kumdhuru mtoto pamoja na mama.
  5. Mtatizo madogo ya ujauzito unayoweza kukumbana nayo unapowahudumia wanawake wajawazito yanaweza kuainishwa kulingana na mifumo ya mwili inayohusika.
  • Matatizo ya utumbo ni kichefuchefu na kutapika, kuchukia baadhi ya vyakula, kiungulio, pika (tamaa ya chakula), uyabisi wa utumbo na hemoroidi.
  • Matatizo ya kiwiliwili cha misuli na ngozi ni maumivu ya mgongo, maumivu kwenye viungo, ugumu wa kuinuka na kujilaza, kuhisi joto au kutokwa na jasho sana, barakoa ya ujauzito (kloasma), maumivu ya kighafla kwenye upande wa sehemu ya chini ya fumbatio, mikakamao mapema katika ujauzito na mikakamao kwenye miguu.
  • Matatizo ya moyo ni uvarikosi na disnia (upungufu wa pumzi).
  • Matatizo ya viungo vya uzazi na vya mfumo wa mkojo ni kukojoa mara kwa mara na mchozo ukeni (unyevunyevu kutoka ukeni).
  • Matatizo ya mfumo wa neva ni kuhisi usingizi na insomnia, maumivu ya kichwa, hisia na mihemko inayobadilika, wasiwasi na hofu, ndoto za ajabu na majinamizi, kusahau, na mabadiliko ya hisia kuhusu ngono.

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 12