13.6.2 Vifaa vya kuzalishia ambavyo mama anapaswa kutayarisha

Vifaa vya kuzalishia ambavyo mwanamke mjamzito na familia yake wanapaswa kushauriwa watayarishe kabla ya kuzaa ni (tazama Mchoro 13.2):

  • Nguo safi kabisa za mama kulalia na za kumpangusa mtoto mzawa na kumfunika
  • Wembe mpya wa kukata kambakitovu
  • Uzi safi mpya wa kufungia kitovu
  • Sabuni, burashi ya kusugua na (ikiwezekana) alkoholi ya tiba ili kutakasa
  • Maji safi ya kunywa, kumwosha mama na mikono yako.
  • Ndoo tatu kubwa au bakuli.
  • Vifaa vya kutengenezea vinywaji vya kuongeza maji mwilini, 'atmit’ au chai.
  • Tochi ikiwa hakuna umeme katika eneo lile.
Mchoro 13.2 Vifaa ambavyo mama anapaswa kutayarisha kwa ajili ya kuzaa.

13.6.1 Kujitayarishia kuzaa kwa njia ya kawaida

13.6.3 Kujiandalia matatizo na kupangia matukio ya dharura