Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 14

Kwa kuwa umekamilisha Kipindi hiki , unaweza kutathmini ni kwa kiwango kipi umeweza kuyatimiza malengo ya masomo ya Kipindi hiki kwa kujibu maswali haya. Yaandike majibu katika shajara yako ya masomo kisha uyajadili na mkufunzi wako katika mkutano saidizi utakaofuata wa masomo. Unaweza kuyalinganisha majibu yako na Muhtasari juu ya Maswali ya kujitathmini mwishoni mwa Moduli hii.

Swali la kujitathmini 14.1 (linatathmini Malengo ya Somo 14.2)

Pendekeza njia za kuwasaidia wanawake ambao hawawezi kumudu vyakula vingi vya aina tofauti jinsi wanavvyoweza kupata kalori za kutosha na aina tofauti za vyakula.

Answer

Maharagwe, ndengu na kunde ni vyakula vya bei nafuu, vyenye virutubishi tele na rahisi sana kukuza. Nyama za viungo kama ini, moyo na figo zina ayoni nyingi na zinaweza kununulika kwa bei nafuu kuliko nyama zingine. Mkate na mchele wa rangi ya kahawia na teff nyeusi huwa na virutubishi zaidi kuliko nafaka za rangi hafifu (isiyoiva) na huwa za bei nafuu ikiwa hawezi kukuza mwenyewe.

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 14.2 (linatathmini Malengo ya Somo 14.1 na 14.2)

Kamilisha Jedwali 14.1. Baadhi ya makundi yameachwa mapengo ya kuandika majibu yako.

Jedwali 14.1 kwa Swali la Kujitathmini 14.2
Kundi la vyakulaVilivyomoMifano mitatu
Vyakula vikuuKabohidrati
Protini
Vyakula vitoavyo nguvu
Vitamini na Madini

Answer

Jedwali lililo hapa chini ni jedwali 14.1 lililokamilishwa. Hatujui hasa ni mifano gani mitatu uliyochagua kwa kila kundi la vyakula, kwa hivyo huenda umetaja mifano mingine mizuri.

Kundi la vyakulaVilivyomoMifano mitatu
Vyakula vikuuKabohidratiInjera, mchele, mahidi, nk
Vyakula vya kukuza (vijenzi)ProtiniMaharagwe, mayai, nyama, nk
Vyakula vitoavyo nguvuSukari na mafutaMatunda, asali, njugu, nk
Vyakula vilinziVitamini na MadiniSamaki, mboga za kijani kibichi, nyama, nk

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 14.3 (linatathmini Malengo ya Somo 14.3, 14.4 na 14.5)

Je, ni ushauri upi unaopaswa kumpa mwanamke mjamzito kuhusu jinsi ya kuepuka maambukizi kwake yeye au kwa mtoto wake mzawa? Fikiria angalau hatua tatu tofauti anazoweza kuchukua.

Answer

Baadhi ya hatua unazoweza kumshauri mwanamke mjamzito kuchukua ili kuepuka maambukizi kwake yeye na kwa mtoto wake mzawa ni:

  • Kunawa mikono yake kwa sabuni hasa kabla ya kutayarisha chakula na baada ya kutumia choo.
  • Kuosha mwili wake kila siku kwa maji safi hasa sehemu yake ya jenitalia.
  • Kuosha meno yake kila siku kwa kijiti cha meno au mswaki.
  • Kupata chanjo dhidi ya tetanasi.
  • Kudumisha usafi na ukavu wa gutu la kiungamwana cha mtoto mzawa hadi litakapoanguka.

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 14.4 (linatathmini Malengo ya Somo 14.1, 14.5 na 14.6)

Je, ni gani kati ya kauli hizi isiyo sahihi? Eleza kisicho sahihi kwa kila kauli.

  • A.Unyonyeshaji hufaa kwa asilimia 100 kwa kuzuia ujauzito mwingine.
  • B.Kolostramu inapaswa kupewa mtoto mzawa bali si kutupwa.
  • C.Kuanza kunyonyesha mapema na bila kumpa mtoto chakula kingine chochote humaamisha kumlisha maziwa ya mama pekee kutoka saa ya kwanza ya maisha ya mtoto hadi angalau umri wa miezi 6.
  • D.Hata kipindi cha hedhi kikirudi wakati wa kunyonyesha bila kumpa mtoto chakula kingine chochote, mwanamke hahitaji kuanza mbinu nyingine ya uzuiaji ujauzito.
  • E.Faida za uzazi wa majira wa angalau miaka 2 ni kupunguza hatari za kifo cha mama na cha fetasi.

Answer

A si sahihi. Kunyonyesha hakufai kwa asilimia 100 katika kuzuia ujauzito mwingine. Kunyonyesha kikamilifu na bila kumpa mtoto chakula kingine chochote hutoa kinga bora dhidi ya ujauzito lakini haiwezi kutegemewa kuwa inayofaa kwa asilimia 100 - hasa baada ya miezi 6 tangu kuzaa au ikiwa kipindi cha hedhi kimerudi.

B ni sahihi. Kolostramu inapaswa kupewa mtoto kwa sababu ina virutubishi vingi na hutoa kinga dhidi ya maambukizi.

C ni sahihi. Kuanza kunyonyesha mapema bila kumpa mtoto chakula kingine chochote humaamisha kumlisha maziwa ya mama pekee kutoka saa ya kwanza ya maisha ya mtoto mpaka angalau umri wa miezi 6.

D si sahihi. Mwanamke anayenyonyesha bila kumpa mtoto chakula kingine chochote hahitaji kuanza mbinu nyingine ya uzuiaji ujauzito iwapo kipindi chake cha hedhi kimerudi.

E ni sahihi. Uzazi wa majira wa angalau miaka 2 hupunguza hatari za kifo cha mama na cha fetasi.

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 14