Malengo ya Somo la Kipindi cha 14

Baada ya kujifunza somo hili unapaswa uweze:

14.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote maalumu yaliyochapishwa kwa herufi nzito (Maswali ya kujitathmini 14.2 na 14.4)

14.2 Kueleza sehemu kuu za mlo kwa afya bora kwa mwanamke mjamzito, kuwashauri wanawake kula vizuri hata wakiwa na fedha chache na ueleze matatizo yatokanayo na lishe duni. (Maswali ya kujitathmini 14.1 na 14.2)

14.3 Kueleza faida za usafi bora na shughuli zingine za kujitunza katika ujauzito (Swali la kujitathmini 14.3)

14.4 Kueleza faida za chanjo dhidi ya tetanasi. (Swali la kujitathmini 14.3)

14.5 Kueleza faida za kuanza unyonyeshaji mapema na pasipo kumpa mtoto chakula kingine chochote kwa mama na kwa mtoto wake. (Maswali ya kujitathmini 14.3 na 14.4)

14.6 Kueleza faida za upangaji uzazi ili kutimiza uzazi wa majira na kujadili uzuiaji wa ujauzito baada ya kuzaa na wanawake wajawazito. (Swali la kujitathmini 14.4)

Kipindi cha 14 Masuala ya Uendelezaji wa Afya Katika Ujauzito

14.1 Lishe katika ujauzito