14.1.1 Kula vizuri

Kula vizuri humaanisha kula vyakula bora vya aina tofauti na pia kula chakula chakutosha. Mchanganyiko huu husaidia mwanamke mjamzito na mtoto wake kuwa wenye afya na nguvu kwa sababu:

  • Humsaidia mwanamke kukingana na maradhi katika ujauzito wake na baada ya kuzaa
  • Hudumisha meno na mifupa ya mwanamke
  • Humpa mwanamke nguvu za kufanya kazi
  • Humsaidia mtoto kukua vizuri kwenye uterasi ya mama
  • Humsaidia mama kurudisha nguvu zake haraka baada ya kuzaa
  • Husaidia katika utengenezaji wa maziwa mengi bora ya mama ili kustawisha mtoto.

Kula vyakula vya aina tofauti

Ni muhimu kwa wanawake wajawazito (kama kila yeyote yule) kula vyakula vya aina tofauti (tazama Picha 14.1): vyakula vikuu (kabohidrati), vyakula vya kukuza au vijenzi (protini), vyakula vilinzi (vitamin na madini), na vyakula vitoavyo nguvu (mafuta na sukari), pamoja na viowevu kwa wingi. Tutaelezea kila mojawapo ya makundi haya kwa kina baadaye katika Kipindi hiki.

Mchoro 14.1 Kula vizuri ni kula vyakula vya aina tofauti ili kupata virutubishi vyote vinavyofaa hasa katika ujauzito na unyonyeshaji na kula chakula cha kutosha kwa afya bora

Kula chakula zaidi

Wanawake wajawazito na wale wanaonyonyesha huhitaji kula zaidi ya kawaida. Chakula cha ziada huwapa nguvu za kutosha na kusaidia watoto wao kukua. Wanahitaji kuongeza chakula wanachokula kikawaida kwa angalau kalori 200 kwa siku au hata zaidi iwapo walikuwa na uzani wa chini kabla ya kupata ujauzito. Kuna njia nyingi za kuongeza chakula cha kila siku kwa kiwango hiki: kwa mfano, kipimo kimoja zaidi cha uji wa mahindi na karanga 12 kwa siku kinaweza kutimiza hitaji hili la ziada.

Wanawake wengine wajawazito huhisi kichefuchefu na kwa hivyo wasipende kula. Hata hivyo, wanawake wajawazito wanahitaji kula chakula cha kutosha - hata wakiwa wagonjwa. Vyakula vya kawaida kama injera au mchele vinaweza kuwa rahisi kwa wanawake hawa kula. Kwa wanawake wanaokumbwa na kichefuchefu, wahimize wale chakula kidogo mara kwa mara.

Matatizo yatokanayo na lishe duni

Lishe duni inaweza kusababisha uchovu, udhaifu, ugumu katika kupigana na maambukizi na matatizo mengine makali ya kiafya. Lishe duni ni hatari hasa katika ujauzito. Inaweza kusababisha kuharibika kwa mimba au mtoto kuzaliwa akiwa mdogo sana au akiwa na kasoro za kuzaliwa. Pia huongeza uwezekano wa mtoto au mama kufariki katika au baada ya kuzaa.

14.1 Lishe katika ujauzito

14.1.2 Kuzungumza na wanawake kuhusu chakula