14.3 Usafi katika ujauzito

Wakati wa ujauzito, wanawake wanapaswa kuwa waangalifu hasa kuhusu usafi wao wa kibinafsi. Wanawake wajawazito hutoa jasho zaidi na hutokwa na mchozo zaidi ukeni kuliko wale wasio wajawazito (kutokana na mabadiliko ya homoni) na wanaweza kuwa wepesi wa kupata maambukizi kutokana na vijidudu vilivyo kwenye mazingira. Kudumisha usafi wa mwili husaidia kuzuia maambukizi. Kuosha mikono kwa sabuni ndilo tendo bora sana analoweza kufanya ili kudumisha usafi hasa kabla ya kutayarisha chakula na baada ya kwenda chooni. Ikiwezekana, mwanamke mjamzito anafaa kuosha mwili wake kwa maji safi kila siku – hasa sehemu ya jenetalia.

Usafi wa meno ni muhimu hasa wakati wa ujauzito kwa sababu viwango zaidi vya estrojeni vinaweza kusababisha kufura na uwezo zaidi wa kupitisha hisi katika tishu za ufizi. Asafishe meno yake kwa kijiti au mswaki na dawa ya meno, mwanake huyo mjamzito anapaswa kufanya hivyo mara kwa mara.

14.2.1 Aina tano muhimu za vitamini na madini

14.4 Kuishi kwa mtindo bora wa maisha