14.6.2 Kanuni za kijumla za kuanza kunyonyesha mapema pasipo kumpa mtoto chakula kingine chochote
Kwa kina mama ambao hawana VVU:
- Watoto wanapaswa kuanza kunyonya mapema iwezekanavyo (hasa katika saa ya kwanza) na kuendelea kwa angalau miezi 6 ya kwanza ya maisha.
- Kolostramu ambayo ndiyo maziwa ya kwanza, inapaswa kupewa mtoto na bali si kutupwa.
- Mtoto anapaswa kunyonyeshwa bila kupewa chakula kingine chochote kwa miezi 6 ya kwanza ya maisha. Mtoto asilishwe wala kunyweshwa kitu kingine chochote katika wakati huu.
- Mtoto anapaswa kunyonyeshwa kila anapotaka, iwe usiku au mchana (anapodai) na hii huchochea matiti kutoa maziwa ya kutosha.
Utajifunza jinsi ya kuwashauri kina mama walio na VVU katika Kipindi cha 16 cha Moduli hii kilicho juu ya uzuiaji wa maambukizi kutoka kwa mama hadi kwa mtoto.
Back to previous pagePrevious
14.6.1 Imani na mazoea duni kuhusu ulishaji wa watoto wazawa