14.7.2 Faida za uzazi wa majira

Kwa kinga kamili, wanawake baada ya kuzaa wasingoje hadi kurudi kwa hedhi ili kuanza mbinu ya kuzuia ujauzito, bali waanze mara tu mwongozo salamu wa mbinu waliyochagua unaporuhusu. (Kanuni zingine za kimsingi za uzuiaji ujauzito baada ya kuharibika kwa ujauzito au kutoka kwa mimba zimeelezwa katika Kipindi cha 20 cha Moduli hii. Majadiliano ya kina juu ya mbinu zote za uzuiaji ujauzito na miongozo vimetolewa katika Moduli ya Upangaji Uzazi katika mtalaa huu.)

Muda wa angalau miaka 2 kati ya uzazi huwa na faida za kiafya kwa mwanamke na mtoto (Kisanduku 14.1).

Kisanduku 14.1 Uzazi wa majira unaofaa hupunguza hatari ya:

  • Kifo cha mama
  • Kifo cha fetasi (kuharibika kwa mimba au kuzaa mtoto mfu), kifo cha mtoto mchanga
  • Anemia kwa mama katika ujauzito utakaofuata
  • Inflamesheni ya bitana ya endometriamu kwenye uterasi baada ya kuzaa
  • Kupasuka kwa mapema kwa membrani za amnioni zinazoizunguka fetasi
  • Kuzaa kabla ya kutimiza muda
  • Ucheleweshaji wa ukuaji wa bitana ya ndani ya uterasi na kuzaa mtoto aliye na uzani wa chini
  • Utapiamlo kwa watoto wazawa na wachanga kutokana na kutopata maziwa ya mama ya kutosha

Linganisha safari zako za huduma za upangaji uzazi na ratiba ya chanjo ya mtoto. Na kumbuka kuwa unyonyeshaji bora hutoa faida mara tatu: uimarikaji wa nafasi za kuishi kwa mtoto na afya yake, afya bora kwa kina mama, na uzuiaji wa ujauzito kwa muda.

Katika Kipindi kitakachofuata, utajifunza kuhusu kanuni za ushauri bora ili uweze kuwasilisha jumbe za uendelezaji wa afya kwa makini kwa wanawake wajawazito wakati wa utunzaji katika ujauzito na kuzungumzia matatizo na imani zao kuhusu ujauzito na kuzaa.

14.7.1 Kunyonyesha na uzuiaji wa ujauzito

Muhtasari wa Kipindi cha 14