Muhtasari wa Kipindi cha 14

Katika Kiako cha 14 ulijifunza kua:

  1. Kula vizuri wakati wa ujauzito na kunyonyesha humaanisha kula aina tofauti za vyakula na vya kutosha - angalau kalori 200 zaidi kila siku.
  2. Kula vizuri ukiwa na pesa kidogo kunawezekana kwa kununua vyakula bora kama maharagwe na nyama za viungo kwa bei nafuu, kukuza jamii kunde, kufuga kuku, kutumia nafaka nzima na kutengeneza supu.
  3. Wanawake wajawazito na wanaonyonyesha wanahitaji kula aina tofauti ya vyakula vikuu (kabohidrati), Vyakula vya kukuza/vijenzi(protini), vyakula vitoavyo nguvu (sukari na mafuta) na vyakula vilinzi (vitamini na madini hasa ayoni, folati, kalisi, aidini na Vitamini A).
  4. Wanamake wajawazito wanapaswa kupewa tembe za ayoni na za folati (asidi ya foliki) kama sehemu ya utunzaji taratibu katika ujauzito.
  5. Usafi wa kibinafsi, hasa kuosha mikono na kudumisha usafi wa sehemu ya jenitalia husaidia kuzuia maambukizi wakati wa ujauzito (na wakati wote).
  6. Kuweza kupumzika na kulala kwa wingi na kuepukana na pombe, sigara, madawa haramu, kemikali kali, na watu wanaoweza kukuambukiza husaidia kumkinga mwanamke mjamzito na mtoto wake ambaye bado hajazaliwa.
  7. Chanjo dhidi ya tetanasi inapaswa kuwa sehemu ya utunzaji taratibu katika ujauzito.
  8. Kumpa mtoto kolostramu na kuendelea kunyonyesha kikamilifu bila kumpa chakula kingine chochote ndiyo lishe bora zaidi na pekee ambayo mtoto huhitaji katika miezi 6 ya kwanza ya maisha.
  9. Kunyonyesha kikamilifu bila kumpa mtoto chakula kingine chochote kunaweza kumkinga mwanamke dhidi ya ujauzito mwingine kwa muda wa hadi miezi 6 baada ya kuzaa lakini ni ikiwa tu unyonyeshaji ni wa mara kwa mara na kipindi chake cha hedhi hakijarudi.
  10. Uzazi wa majira wa angalau miaka 2 ni bora kwa afya ya mwanamke, mtoto wake na watoto wowote wakubwa alionao – kwa hakika kwa jamii yote.

14.7.2 Faida za uzazi wa majira

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 14