Maswali ya kujitathmini ya Kipindi cha 15

Kwa kuwa umekamilisha kipindi hiki, unaweza kutathmini jinsi ulivyoafikia Malengo yake ya Mafunzo kwa kujibu maswali yafuatayo. Andika majibu kwenye shajara yako na kuyajadili na mkufunzi wako katika mkutano utakaofuata wa masomo. Unaweza kulinganisha majibu yako na muhtasari kuhusu Maswali ya Kujitathmini mwishoni mwa Moduli hii.

Swali la kujitathmini 15.1 (linatathmini Malengo ya Somo 15.1 na 15.2)

Kwa kila kauli, onyesha ikiwa ni kweli au la. Eleza kisicho sahihi kwa kauli yoyote ambayo si kweli.

  • A.Kusema karibu, kutabasamu, kumhimiza kueleza wasiwasi na shaka alizo nazo humsaidia mama kutulia na kuwa na imani nawe.
  • B.Lazima umweleze kuwa asipokuja siku aliyoratibiwa, hutamhudumia wakati mwingine wowote.
  • C.Usimruhusu kuuliza maswali hadi utakapomaliza kumweleza anachofaa kujua.
  • D.Unaweza kumshauri mwanamke mmoja aliyekaa nawe huku ukiendelea kumfanyia yule mwingine uchunguzi.
  • E.Akikuambia kuwa binti zake wawili walipashwa tohara siku alipo zalia nyumbani, mwambie kwa ukali kuwa asifanye hivyo tena na ikiwa anapanga kurudia hayo kwa mtoto huyu iwapo ni wa kike, asirudi tena kwa safari zingine zozote.
  • F.Kumshauri mwanamke mjamzito kuhusu dalili za hatari ni muhimu katika kila safari.

Answer

A ni kweli. Kumkaribisha mama, kutabasamu na kumhimiza kueleza wasiwasi na shaka alizonazo humsaidia kutulia na kuwa na imani nawe.

B si kweli. Si jambo rahisi kwa wengi wa wanawake wajawazito chini mwa Sahara kuja siku waliyoratibiwa, hasa kutokana na majukumu yao mengi ya kibinafsi na ya kijamii. Ni haki yao kuja kabla au baada ya siku waliyoratibiwa, au hata wasije kabisa. Ni wajibu na jukumu la mtaalam yeyote wa afya kuwakaribisha kwa mkono mkunjufu siku au wakati wowote ule watakapokuja kwa uchunguzi.

C si kweli. Huduma ya afya kimsingi ni haki ya mteja/mgonjwa. Wajibu wa wataalam wa afya ni kutoa huduma ya kumtuliza na kumridhisha. Kwa hayo, unafaa kujitayarisha kuulizwa maswali na kufanya juhudi kuwahimiza wanawake kuuliza maswali wasiyoelewa.

D si kweli. Kwa kanuni zake, utoaji ushauri ni kujadili maswala ya kibinafsi ambayo mteja hatapendelea yakijadiliwa na yeyote nje ya familia. Kwa hivyo, hata ukiwa na haraka, si vyema kumshauri mwanamke mmoja huku ukimchunguza mwingine. Katika mazingira kama hayo, anayeshauriwa hataweza kueleza hisia na wasiwasi wake kwa uwazi kwako.

E si kweli. Huwezi kuhimiza mabadiliko ya kitabia kwa watu wazima kwa kukosoa vikali, kuwapinga, kuwavunja moyo na kuwakatisha tamaa wazi wazi. Mwanamke huyu hatahisi kuheshimiwa na huenda asirudi kwa huduma zaidi ya utunzaji katika ujauzito. Ili kuleta mabadiliko bora kwa mienendo duni, mbinu bora zaidi kwa watu wazima ni majadiliano ya wazi ukiwajuza hatari/hasara na kuwapa fursa ya kukadiria chaguzi walizonazo wenyewe na kufanya uamuzi wao.

F ni kweli. Katika kila safari ya huduma katika ujauzito, wanawake wajawazito wanafaa kupewa ushauri kuhusu dalili za hatari katika ujauzito ili waweze kuchukua hatua ya haraka kunapotokea dharura.

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 15.2 (linatathmini Lengo la Somo 15.3)

Kutokana na uliyosoma katika Jedwali 15.1, linganisha kila dalili ya hatari na hali mwafaka ya kiafya.

Using the following two lists, match each numbered item with the correct letter.

  1. Kuvuja kwa kiowevu ukeni

  2. Kutokwa na damu ukeni

  3. Joto jingi

  4. Kupungua kwa ukubwa wa fumbatio

  5. Maumivu kwenye fupanyonga

  6. Maumivu ya kichwa yanayodumu

  • a.Utokaji potelelevu

  • b.Pielonefritisi kali

  • c.Malaria

  • d.Upasukaji wa mapema wa membreni

  • e.Hipatensheni

  • f.Kutokwa na damu kabla ya kuzaa

The correct answers are:
  • 1 = d
  • 2 = f
  • 3 = c
  • 4 = a
  • 5 = b
  • 6 = e

Swali la kujitathmini 15.3 (linatathmini Lengo la Somo 15.4)

Kwa kila kauli, eleza ikiwa ni kweli au la. Eleza kisicho sahihi kuhusu kila kauli isiyo kweli.

  • A.Mshauri anastahili kumweleza mwanamke mjamzito kuhusu dalili zote za hatari za ujauzito katika safari yake ya kwanza ya utunzaji katika ujauzito kabla ya majuma 16 ya ujauzito.
  • B.Kumhimiza mwanamke mjamzito kurudia yaliyojadiliwa katika ushauri kutaongeza kumbukumbu yake (uwezo wa kuendeleza kuwepo) ya hoja muhimu.

Answer

A sikweli. Kipengele wanachohitaji kushauriwa kukihusu kinafaa kulingana na umri wa ujauzito kwa sababu:

  • Matatizo tofauti yanayohusiana na ujauzito hutokea katika vipindi tofauti vya ujauzito.
  • Si rahisi kwa wateja kuelewa na kuhifathi habari nyingi hasa isipokuwa muhimu kwao wakati huo.
  • Kuongea kuhusu dalili zote za hatari katika safari moja kutachukua wakati wako mwingi.
  • Habari nyingi zaidi kuhusu hatari inayoweza kutisha inaweza kuwazidi wateja na kuwazuia kuuliza maswali yao na ufafanuzi.

B ni kweli. Kurudia yaliyojadiliwa/yaliyosemwa kutasaidia:

  • Mwanamke mjamzito kukumbuka alichosikia.
  • Mhudumu wa afya kuchunguza kiwango cha kuelewa cha mwanamke huyo.

Mwisho wa jibu

Swali la kujitathmini 15.4 (linatathmini Lengo la Somo 15.5)

Orodhesha manufaa ya kumhusisha mume/mwenzi katika ushauri wa kabla ya kuzaa kuhusu dalili za hatari.

Answer

  • Kumshauri mume/mwenzi kuhusu dalili za hatari katika safari za huduma ya utunzaji katika ujauzito inamaanisha kuwa hata yeye anaweza kuzimakinikia na kutafuta usaidizi wa haraka wakati wa dharura.
  • Kuwahusisha waume/wenzi ni njia moja ya kujulisha wana nchi kwa upana kuhusu hatari zinazoweza kuwakumba wanawake na watoto katika ujauzito.
  • Ikiwa mume/mwenzi atajua dalili zinazoweza kutokea katika ujauzito, anaweza kujali zaidi na kuhusika kwa kumtunza mkewe.
  • Ana uwezekano mkubwa wa kukubali kumpeleka mkewe mjamzito kwa mhudumu wa afya ikiwa dalili za hatari zitaibuka.
  • Kumshauri mume/mwenzi kutamuwezesha kujiandaa kisaikolojia na kifedha kukabiliana na dharura zinazohusiana na ujauzito.

Mwisho wa jibu

Maswali ya kujitathmini 15.5 (yanatathmini Malengo ya Somo 15.1 hadi 15.5)

Soma kwanza Uchunguzi Maalum 15.1 kwa makini kisha ujibu maswali yanayofuata.

Uchunguzi maalum 15.1 Kisa cha Bi. H

Bi. H ni mwanamke mwenye umri wa miaka 25 aliye katika ujauzito wa pili na alimtembelea mhudumu wa afya nje ya hospitali kwa mara ya kwanza baada ya majuma 34 ya ujauzito. Mhudumu huyo wa afya aliuliza mahali alikozalia awali. Shinikizo la damu na uzani vilipimwa na afya yake ilionekana kuwani njema; fumbatio lake lilichunguzwa na ujauzito kuonekana kuendelea kikawaida. Mwisho, aliagizwa kurudi baada ya majuma 3.

Majuma mawili baadaye, alianza kuvuja kiowevu cha majimaji ukeni. Aliwajulisha jirani zake na wakamwambia asihofu. Kwa kuwa kiliendelea kuvuja, siku ya tatu baada ya kuanza kuvuja, alimrudia mhudumu huyo wa afya na kupata ushauri huo huo alioupata nyumbani. Siku ya tano, alipata joto jingi sana (sentigredi 39) na kiowevu kinachonuka kutoka ukeni.

  • a.Je, nini kibaya na safari ya huduma ya utunzaji katika ujauzito baada ya majuma 34 ya ujauzito kwa mtazamo wa kumshauri mwanamke mjamzito ipasavyo?
  • b.Je, kwa nini Bi. H alivuja kiowevu ukeni?
  • c.Je, kwa nini alingoja siku tatu kabla ya kuripoti kwa mhudumu wa afya nje ya hospitali baada ya kuanza kuvuja?
  • d.Je, nini ambacho kingefanywa na mhudumu wa afya nje ya hospitali Bi. H alipowasili akivuja kiowevu ukeni?
  • e.Je, kwa nini Bi. H alipata kiwango cha juu sana cha joto na kiowevu kinachonuka ukeni?

Answer

  • a.Bi. H hakushauriwa kuhusu dalili za hatari za ujauzito katika umri wa majuma 34 ya ujauzito. Alipokuwa na wasiwasi kuhusu dalili alizokuwa nazo aliomba ushauri kutoka kwa majirani. Walifikiri (bila usahihi) kuwa kuvuja kiowevu cha majimaji ukeni katika juma la 36 ilikuwa ni kawaida kuliko matatizo mabaya yanayohusiana na ujauzito.
  • b.Kiowevu cha majimaji kilivuja kutokana na kupasuka kwa mapema kwa membreni za fetasi ambazo ndizo kifuko kinachoweka fetasi na kiowevu cha amnioni. Kwa hivyo ni kiowevu cha amnioni kilichokuwa kikivuja kupitia membreni zilizopasuka.
  • c.Alingoja siku kadhaa kabla ya kutafuta usaidizi kwa sababu hakujua kuwa kuvuja kwa kiowevu ni dalili ya hatari ya kupasuka kwa mapema kwa membreni na majirani walimhakikishia kuwa si tatizo.
  • d.Mhudumu wa afya nje ya hospitali angempa rufaa aende katika kituo cha afya au hospitali kwa uchunguzi na matibabu.
  • e.Bi. H alipata kiwango cha juu sana cha joto na mchozo unaonuka kutoka ukeni kwa sababu maambukizi yaliweza kupanda ukeni hadi kwenye uterasi baada ya kupasuka kwa membreni.

Mwisho wa jibu.

Muhtasari wa Kipindi cha 15