Malengo ya Somo la Kipindi 15

Baada ya kipindi hiki, unafaa uweze:

15.1  Kueleza na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyoandikwa katika herufi nzito. (Swali la kujitathmini 15.2)

15.2  Kujadili kanuni za kijumla za kutoa ushauri na kutoa muhtasari wa ujuzi na mitazamo ya mshauri bora. (Maswali ya kujitathmini 15.1, 15.3, 15.4 na 15.5)

15.3  Kueleza umaalumu wa kuwashauri wanawake wajawazito. (Maswali ya kujitathmini 15.1 na 15.3)

15.4  Kueleza dalili za hatari zinazotokea sana zinazoweza kuhisiwa au kutambuliwa na wanawake wajawazito, umri wa ujauzito ambapo kila dalili ina uwezekano mkubwa wa kutokea, na hatua ambayo mwanamke huyo anafaa kuchukua (Maswali ya Kujitathmini 15.2 na 15.5)

15.5  Kutambua wakati bora wa kutoa ushauri kuhusu aina tofauti za dalili za hatari kwa mujibu wa umri wa ujauzito. (Swali la kujitathmini 15.3)

15.6  Kueleza umuhimu wa kumhusisha mume au mwenzi katika ushauri kwa wanawake wajawazito kuhusu dalili za hatari. (Swali la kujitathmini 15.4)

Kipindi cha 15 Kuwashauri Wanawake Wajawazito kuhusu Dalili za Hatari

15.1  Kanuni za kijumla katika ushauri wa mwanamke mjamzito