15.1  Kanuni za kijumla katika ushauri wa mwanamke mjamzito

Kumshauri mwanamke mjamzito ni mawasiliano ya njia mbili kati ya watu wawiliambapo unamsaidia kujua kuhusu matatizo yanayoweza kumkumba katika ujauzito na kisha afanye uamuzi wake wa jinsi ya kuyatatua. Mnapoanza majadiliano haya mkiwa mmefahamiana vyema haimsaidii tu mwanamke huyo kujua matatizo yanayoweza kumkumba, bali pia hujenga uaminifu kati yenu. Pia, njia hii ya mawasiliano humtuliza mwanamke huyo na kumwezesha kuwasilisha wasiwasi na matakwa yake kwako akiwa huru.

Kumbuka kuwa mwanamke mjamzito ni mtaalam pia katika matakwa na hali yake. Amejifunza mengi Kivyake (wakati mwingine sahihi na mwingine yasiyo sahihi). Kwa hivyo, usimpinge kuwasilisha kwako imani na mawazo yake kutoka mwanzo - unafaa kustahimili imani na maadili ya kila mwanamke huku ukijaribu kuondoa kwa upole na kimakini mambo yoyote potovu sana anayoweza kuwa nayo. Heshima na ustahimilivu kwa imani potovu haimaanishi kuwa unazikubali na haziwezi kubadilishwa. Umakini na ustahimilivu ni mbili za sifa bora bainifu za mshauri bora.

Kisanduku 15.1 kinatoa muhtasari wa ujuzi na mitazamo unayohitaji ili kuanzisha mawasiliano bora na mteja yeyote, wakiwemo wanawake wajawazito. Mchakato wa kushauri hupitia awamu hizi: kujenga uhusiano na wanawake wajawazito, kuchunguza matatizo yao, kuwezesha mbadilishano wa habari na kutamatisha mchakato huu wa mashauriano kwa furaha na miadi.

Mchoro 15.1   Kudumisha usiri hujenga uaminifu.

Kisanduku 15.1  Ujuzi na mitazamo kwa mawasiliano bora ya njia mbili

  • Mkaribishe mwanamke na aketi karibu nawe akikutazama.
  • Tabasamu na muweze kuangaliana ana kwa ana.
  • Mhakikishie tena kuwa mtakayozungumza yatawekwa siri (Mchoro 15.1).
  • Usihusishe mtu wa tatu kwenye mkutano huu bila idhini yake.
  • Tumia lugha rahisi isiyo ya kitabibu wakati wote ili aweze kuelewa na uhakikishe mara kwa mara kuwa ameelewa.
  • Msikize kwa makini kwa kutumia ishara na kuzungumza ili kuonyesha kuwa unasikiza yote anayoyasema.
  • Mhimize aulize maswali, aeleze matakwa na shaka alizonazo na kuuliza asipoelewa.
  • Kikawaida anafaa kuongea kwa theluthi mbili za muda wote nawe uzungumze theluthi moja (tazama Mchoro15.2). Utafiti umeonyesha kuwa wataalamu wa afya mara nyingi huongea sana badala ya kuwapa wateja muda wa kutosha wa kutoa maoni na matakwa yao.
Mchoro 15.2 Wahudumu wa afya wanapaswa kuongea kwa muda mfupi na kuwahimiza wateja wao kuongea zaidi.

Malengo ya Somo la Kipindi 15

15.2  Je, nini cha muhimu kuhusu kuwashauri wanawake wajawazito?