15.2  Je, nini cha muhimu kuhusu kuwashauri wanawake wajawazito?

Kwa mwanamke mjamzito, kusudi la kijumla la kupata ushauri ni kumpa habari muhimu kwa kuendeleza au kudumisha afya yake pamoja na ya mtoto wake kabla na baada ya kuzaa. Mahususi, ushauri utamsaidia mwanamke mjamzito kuishi mwenye afya kwa kumshauri kuhusu masuala ya uendelezaji wa afya kama vile lishe (ulijifunza haya katika Kipindi cha 14) na pia kujua dalili zitokeazo sana za hatari za kiafya zinazoweza kumdhuru yeye na mtoto wake. Mbali na haya, ushauri ni kiingilio kwenye familia hasa kwa mume/ mwenziwe ili pia wajue hatari zinazoweza kutokea katika ujauzito na kujitayarisha kisaikolojia na kiuchumi. Kisanduku 15.2 kinatoa muhtasari wa matokeo bora ushauri kuhusu dalili za hatari katika kipindi cha ujauzito.

Mchoro 15.3  Ikiwa mwanamke mjamzito atakuamini, anauwezekano wa kuja na kupata huduma ya utunzaji kabla ya kuzaa.

Kisanduku 15.2  Kushauri kuhusu dalili za hatari

Kushauri kumefanikiwa ikiwa mwanamke mjamzito:

  • Anahisi amepata usaidizi aliohitaji.
  • Anaelewa dalili za hatari zinazotokea sana.
  • Anajua la kufanya na kujihisi mjasiri kuwa anaweza kuja karibuni apatapo mojawapo ya dalili za hatari.
  • Anahisi kuheshimiwa, kusikizwa na kuthaminiwa.
  • Atarudi anapohitaji usaidizi wako (anakuamini, tazama Mchoro 15.3)

15.1  Kanuni za kijumla katika ushauri wa mwanamke mjamzito

15.3  Je, dalili za hatari zitokeazo sana katika ujauzito ni zipi?