15.3  Je, dalili za hatari zitokeazo sana katika ujauzito ni zipi?

Kutokea kwa dalili hizi za hatari zinazoweza kuhisiwa au kugunduliwa na mwanamke mjamzito hutofautiana kulingana na umri wa ujauzito.

  • Je, ni nini maana ya trimesta ya kwanza, ya pili na ya tatu ya ujauzito?

  • Trimesta humaanisha ‘kipindi cha miezi mitatu’. Trimesta ya kwanza ni miezi mitatu ya kwanza ya ujauzito (yaani, tangu utungaji mimba hadi mwisho wa juma la 14 la ujauzito, muda huo ukipimwa tangu kipindi chake cha mwisho cha kawaida cha hedhi); trimesta ya pili ni kutoka miezi 3 hadi 6 (yaani, kuanzia majuma 15 hadi 27); trimesta ya tatu ni miezi 3 ya mwisho ya ujauzito (yaani, kuanzia majuma 28 hadi kuzaa ambapo ni hata hadi baada ya majuma 42).

    Mwisho wa jibu

Tayari umejifunza kuhusu uchunguzi wa matatizo yanayohusiana na ujauzito na afya kwa kuchukua historia ya mwanamke na kufanya uchunguzi wa kimwili (kumbuka Vipindi vya 8 na 9). Hata hivyo, unaweza tu kutambua hatari za kiafya kwa mama au mtoto katika uchunguzi wa ujauzitoni, kwa hivyo ni muhimu kumsaidia mama kutambua dalili zozote kivyake na kujua anapopaswa kuja kwako haraka.

Kwanza unahitaji kujua vizuri sana wakati ambapo matatizo yanayohusiana na ujauzito au ya kiafya hutokea kwa kuchukua umri wa ujauzito kama muda muhimu (tazama Jedwali 15.1). Pili, unapaswa kuwa makini usije ukampa mwanamke huyo habari nyingi kwa wakati mmoja. Tatu, kumbuka kuwa utoaji wa ushauri si tukio la wakati mmoja - unafaa kuwa tayari kurudia ujumbe kuhusu dalili za hatari kila unapomhudumia na kuhakikisha kuwa ameelewa vizuri.

Tayari unajua kuhusu baadhi ya matatizo yaliyoorodheshwa katika Jedwali 15.1 ( k.m ujauzito wa nje ya uterasi na ujauzito bandia). Baadaye katika Moduli hii, utajifunza kwa kina kuhusu visababishi vingine vya vifo vya kina mama na vya fetasi, na kuugua katika ujauzito: hiparemisisi gravidaramu ilikuwa katika Kipindi cha 12; urarukaji wa mapema wa membreni umejadiliwa katika Kipindi cha 17; malaria, anemia, na maambukizi ya mfumo wa viungo vya mkojo yamejadiliwa katika Kipindi cha 18, maradhi ya kihipatensheni ya ujauzito yako katika Kipindi cha 19; kuharibika kwa ujauzito na utokaji wa ujauzito, na kutokwa na damu ukeni mwanzoni na mwishoni mwa ujauzito yako katika Vipindi vya 20 na 21 mtawalia.

Uchungu wa mara kwa mara kwenye sehemu ya chini ya fumbatio pekee hutokea sana mwanzoni mwa ujauzito na kivyake si dalili ya hatari.

Jedwali 15.1  Dalili za hatari katika ujauzito

Dalili ambazo mama hupitia

(maneno yaliyo katika herufi za mlazo ndiyo muhimu sana)

Huenda akawa na hali hii ya kiafya
Utungaji mimba hadi majuma 20 ya ujauzito
Kutapika kunakodumu, kupoteza uzito

Hiparemesisi gravidaramu

Inayoonyeshwa kwa kutapika mara kwa mara, kupoteza kilo 5 au zaidi za uzani, uchunguzi wa mkojo unaonyesha ketoni 2+ au zaidi (Ulisoma haya katika Kipindi cha 12; jinsi ya kufanya uchunguzi wa mkojo katika Kipindi cha 19)

Kutokwa na damu (mbichi) ukeni, huenda ikawa na madonge ya damu au nyama, na uchungu kwenye sehemu ya chini ya fumbatio Utoaji mimba (kali)

Aina zote za uharibikaji wa ujauzito ni matukio makali na ya ‘ghafla’ isipokuwa utoaji potelelevu (Utasoma kuhusu utoaji katika Kipindi cha 20

 
Dalili za ujauzito zinapotea, fumbatio halikui au hata linapungua kwa ukubwa, huenda kukawa na kuvuja kwa damu nzito

Utoaji potelelevu

Fetasi au tishu ya fetasi inapokuwa kwenye uterasi wakati hakuna ishara za uhai na seviksi imefungwa kabisa

 
Kuvuja damu ukeni, (kama vile hedhi), maumivu kwenye sehemu ya chini ya fumbatio, kukosa hedhi au hedhi isiyo ya kawaida

Ujauzito wa nje ya uterasi

(umeangaziwa katika Vipindi vya 5 na 12)

Kutokwa na damu ukeni

 Kutokwa na damu (mbichi), kupita kwa tishu zinazofanana na barafu iliyochafuliwa kwa damu (tishu zinazofanana na zambarau), ukuaji wa haraka wa fumbatio

Ujauzito bandia

 

 (imejadiliwa katika Vipindi vya 10 na 20)

Umri wa majuma 20 hadi mwishoni mwa ujauzito
Maumivu ya kichwa, hisia ya kuungua kwa epigastriamu (Mchoro 15.4) kiwaa, Kuvimba kwa mwili (kunakohusisha mgongo, ukuta wa fumbatio, mikono na uso), kupungua kwa kiasi cha mkojo

Matatizo ya kihipatensheni ya ujauzito (Priklampsia na eklampsia yalitangulizwa katika Vipindi vya 8 na 9, utajifunza zaidi katika Kipindi cha 19) 

Mchoro 15.4

Kutokwa na damu ukeni mwishoni mwa ujauzito, hata kiasi kidogo

Kuharibika kwa mimba mwishoni mwa ujauzito (majuma 20 hadi 27) au kutokwa na damu katika ujauzito (majuma 28 na zaidi) (Utajifunza zaidi katika Kipindi cha 20)
Kuvuja kwa viowevu vya majimaji kutoka ukeni na kulowesha chupi zake pakubwa na kunaweza kukithiri

Upasukaji wa mapema wa membreni

(Utajifunza kuhusu urarukaji wa mapema wa membreni katika Kipindi cha 17)

Kuongezeka kunakoendelea kwa maumivu yanayosukuma chini kwenye sehemu ya chini ya fumbatio kabla ya miezi 9 ya ujauzito

Leba ya mapema

(Imeangaziwa katika Moduli ya Utunzaji katika Leba na Kuzaa)

Hakuna mabadiliko katika ukuaji wa fumbatio, kusonga kwa fetasi kunasikika chini ya mara kumi kwa saa 12. (Idadi yoyote ya kusonga kwa fetasi kwa dakika moja, huhesabiwa kama moja)Vizuizi dhidi ya ukuaji wa fetasi kwenye uterasi (Imeangaziwa kwa kifupi katika Kipindi cha 7)

Fetasi kukosa kusonga kwa zaidi ya saa 6

Fetasi kufia ndani ya uterasi

Wakati wowote katika ujauzito

Kiwango juu cha joto, maumivu ya kichwa, kutetemeka, kuhisi baridi, kutokwa na jasho, kuhisi kiu, kuhisi maumivu kwa mwili wote, kukosa hamu ya kula

Malaria, kipindupindu, homa ya chawa au homa ya vipindi

(Utajifunza kuhusu maambukizi haya katika Moduli ya Magonjwa ya kuambukiza)

Mchoro 15.5 Maambukizi katika sehemu hii ya figo husababisha dalili za hatari.

Kukojoa kwa mara kwa mara kwenye uchungu na, na huenda mkojo ukawa na damu au uwe kama usaha

Maambukizi ya mfumo wa viungo vya mkojo (Maambukizi ya mfumo wa viungo vya mkojo, uvimbe wa kibofu au urethraiti)

(Utajifunza kuhusu maambukizi ya mfumo wa viungo vya mkojo katika Kipindi cha 18)

Maumivu mbavuni, joto jingi, kutapika, mkojo wenye damu, kukazwa na kukojoa mara kwa mara

Pielonefritisi (Inflamesheni ya figo) kali (Mchoro 15.5 unaonyesha sehemu maalum kwenye figo ambapo maambukizi haya yanaweza kutokea)

Macho kuwa na rangi ya manjano, kukosa hamu ya kula, kuchukia harufu ya vyakula vyenye vikolezo, anahisi uchovu kichefuchefu, na kutapika

Ugonjwa wa ini

Anahisi kiu, anakunywa maji mengi, anakojoa mara kwa mara, anahisi njaa, kupoteza uzani kwa mfululizo,

Kisukari Melitasi

Kukohoa

Ugonjwa wa mapafu na moyo

Jedwali 15.1 ni muhtasari wa kina unaofaa kusoma kama mhudumu wa afya. Haitakuwa bora wala muhimu kumuonyesha mwanamke mjamzito katika safari za utunzaji katika ujauzito.

  • Je, unaweza kueleza ni kwa nini sivyo?

  • Jedwali hili linatumia lugha ya kitiba ambayo huenda mwanamke asielewe (ila naye pia ni mhudumu wa afya), na inaweza kumjaza kwa habari nyingi zaidi kwa wakati mmoja na kumpa wasiwasi wa kutazamia hatari nyingi zinazoweza kumkumba yeye na mtoto wake.

    Mwisho wa jibu

Jedwali 15.2 ni muhtasari uliorahisishwa na kuwekwa katika sehemu mbili unaoweza kujadiliwa na wanawake wajawazito katika kipindi kinachofaa cha ujauzito. Wanawake walio katika awamu ya kimsingi ya utunzaji katika ujauzito, ulioelezwa katika Kipindi cha 13, wanafaa kuhudumiwa kwa safari ya kwanza kabla ya majuma 16 ya ujauzito, na kwa safari ya pili kati ya majuma 20-24). Hakikisha kuwa kila mwanamke anajua dalili za hatari zinazotokea sana katika ujauzito zilizo na uwezekano mkubwa wa kutokea katika kila kipindi.

Jedwali 15.2 Dalili za hatari ambazo kila mwanamke mjamzito anafaa kujua.
Katika safari zote kabla ya majuma 20Safari zote baada ya majuma 20

Kutapika mara kwa mara

Kutokwa na damu ukeni

Hakuna mabadiliko katika ukuaji wa fumbatio

Joto jingi

Kutapika

Maumivu ya kichwa

Hisia ya kuungua kwa epigastrimu (tazama Mchoro 15.4)

Kiwaa

Kutokwa na damu ukeni

Kuvuja kwa kiowevu

Hakuna mabadiliko katika ukuaji wa fumbatio

Kutapika mara kwa mara

15.2  Je, nini cha muhimu kuhusu kuwashauri wanawake wajawazito?

15.4 Kuwaeleza wanawake wajawazito kuhusu dalili za hatari