15.4 Kuwaeleza wanawake wajawazito kuhusu dalili za hatari

Unafaa kufahamu kuwa wanawake wajawazito wanayo majukumu mengi nyumbani, hasa mashambani na huenda wakawa wamejazwa na habari nyingi kuhusu ujauzito huu. Jedwali 15.2 linawasilisha mambo ambayo mama anastahili kujua kwanza, lakini kamwe usimweleleze kila kitu kwa wakati mmoja. Kumshauri mwanamke mjamzito kulingana na vipindi vya ujauzito ni mkakati unaofaa kutokana na mtazamo wa uelewaji wa mwanamke huyo na utumiaji wa muda wako ifaavyo. Yaani, unafaa kujadiliana naye dalili za hatari zinazotokea sana, kwa kuzingatia kipindi cha ujauzito. Kwa mfano, mwanamke anayekuja kwa ajili ya utunzaji katika ujauzito kabla ya umri wa majuma 20 ya ujauzito anafaa kushauriwa kuhusu dalili za hatari za kuharibika kwa ujauzito zinazojitokeza kwa kutoka kwa damu ukeni. Pia anafaa kujua dalili za hatari za matatizo ya kiafya yanayotokea sana yanayoweza kutokea wakati wowote katika ujauzito - kama vile yanavyoweza kutokea kwa mtu yeyote.

Matatizo mengi makali yanayohusiana na ujauzito hutokea katika trimesta ya tatu. Kwa hivyo, ni wakati mzuri wa kumshauri mama kuyahusu katika trimesta ya pili ili kumpa muda wa kujiandaa mapema. Unaweza kutumia maagizo yaliyochapishwa, michoro, picha ukiwa nazo, kwani zinaweza kumsaidia kuelewa na kuongeza uwezo wake wa kukumbuka mambo muhimu. Hii ni njia bora ya kumkumbusha kuhusu mlichojadili katika safari za utunzaji katika ujauzito hapo awali (tazama Jedwali 15.3).

Kisanduku 15.3 Kufuatilia ujumbe wa ushauri wa awali

Katika safari zitakazofuata za huduma ya ujauzitoni, kumsaidia mwanamke kupitia mliyoyajadili awali kutakusaidia:

  • Kutambua alivyoelewa swala hili
  • Kutambua anayoweza kukumbuka kwa usahihi
  • Kujua ikiwa amekubali na yuko tayari kutumia maarifa hayo
  • Kujua sehemu alizoelewa vibaya

Pia, kutamsaidia kueleza shaka na hofu alizonazo, ili muweze:

  • Kujadili maswala yoyote ambayo hayakueleweka au kupokelewa vyema
  • Kupanga kwa pamoja mtakachofanya, kwa kumhusisha mume/mwenziwe.

15.3  Je, dalili za hatari zitokeazo sana katika ujauzito ni zipi?

15.5 Umuhimu wa kumhusisha mume/mwenzi katika ushauri wa ujauzitoni