15.5 Umuhimu wa kumhusisha mume/mwenzi katika ushauri wa ujauzitoni

Matatizo mengi yanayohusiana na ujauzito hayawezi kutabirika na hutokea baadaye. Kwa upande mwingine, ufahamu wa wana nchi kuhusu hatari za kiafya kwa mama na fetasi zinazohusiana na ujauzito ni mdogo sana. Chini mwa Sahara, mume au mwenzi wa kiume huwa na ushawishi mkubwa, uwezo wa kiuchumi na kukubalika kijamii kuliko mwanamke. Kuwashauri wanawake wajawazito wengi iwezekanavyo ni njia moja ya kuufikia umma kwa kumhusisha mumewe ambaye anaweza kuwa ajenti wa pili kwa usambazaji wa hatari zinazoweza kutokea katika ujauzito kwa umma.

Kwa hivyo, kumhusisha mume/mwenzi katika safari za utunzaji katika ujauzito kuna manufaa mengi (Kisanduku 15.4).

Kisanduku 15.4 Kumhusisha mume/ mwenzi katika safari za huduma katika ujauzito

  • Humsaidia mwenzi/mume kujua dalili za hatari ambazo mwanamke anaweza kupata katika ujauzito.
  • Kutamfanya awe mwenye kujali zaidi na kujihusisha.
  • Humsaidia kuchukua hatua (kuripoti mapema) dalili za hatari zinapotokea.
  • Hummakinisha kuweka akiba ya pesa kwa uwezekano wa dharura, kwa mfano kumsafirisha hadi kwenye kituo cha afya.
  • Huimakinisha familia kuamua pahali wanapopendelea pa kuzalia.
  • Huisaidia familia kujiandaa kumtunza mama na mtoto wake baada ya kuzaa.
  • Ni hatua zaidi ya kuongeza ufahamu wa wana nchi kuhusu hatari zinazoweza kutokea katika ujauzito.

15.4 Kuwaeleza wanawake wajawazito kuhusu dalili za hatari

15.6 Orodha ya kukagulia baada ya kila kipindi cha ushauri katika ujauzito