15.6 Orodha ya kukagulia baada ya kila kipindi cha ushauri katika ujauzito

Mwisho, tunatamatisha kipindi hiki kwa orodha ya kukagulia unayoweza kutumia kutathmini ujuzi na mitazamo yako ya utoaji ushauri (Jedwali 15.3). Imechukuliwa ili kutumika katika kuwashauri wanawake wajawazito, bali inashirikisha kanuni za kijumla za kutoa ushauri unazoweza kutumia kwa mteja yeyote aliye chini ya utunzaji wako wa kiafya.

Jedwali 15.3 Oroaha ya kukagulia ya ‘KUSANYA’ ujuzi wa kutoa ushauri (imerekebishwa kwa wanawake wajawazito).
SalimuJe:

Ulimkaribisha kila mwanamke mjamzito alipowasili?

Mlijadiliana mahali penye starehe na faraghani?

Ulimhakikishia mwanamke mjamzito usiri wa mtakayo ya zungumza?

Ulionyesha kujali na kumpokea kwa maneno na ishara katika mkutano?

Ulieleza cha kutarajiwa?

UlizaJe:

Ulimwuliza mwanamke huyo mjamzito sababu ya safari hii?

Ulimhimiza mwanamke huyo mjamzito kuongea theluthi mbili za maongezi?

Uliuliza maswali ‘wazi’ kwa wingi?

Ulimakinikia yaliyosemwa na mteja huyo na jinsi yalivyosemwa?

Ulijiweka katika nafasi ya mwanamke huyo — ukionyesha kuelewa aliyoyasema bila kumkosoa vikali wala kumhukumu?

Uliuliza anavyohisi?

Uliuliza kuhusu mapendeleo yake?

Je:

Ulianza majadiliano kwa kuzingatia mapendeleo ya mwanamke mjamzito?

Ulijadili dalili za hatari za ujauzito kulingana na umri wa ujauzito?

Ulitoa habari kuhusu dalili za hatari za ujauzito ili kumsaidia kufanya uamuzi wake mwenyewe?

Uliepuka kumpa habari nyingi zaidi kwa wakati mmoja?

Ulitumia maneno anayoweza kuelewa?

Ulijadili umuhimu wa kuripoti mapema ikiwa atakumbana na dalili za hatari katika ujauzito?

UsaidiziJe:

Ulimjulisha kuwa uamuzi ni wake?

Uliwasaidia wanawake wajawazito kuweza kutambua dalili za hatari zinazotokea sana?

Ulimsaidia kuweza kuwazia athari kwa maisha yake na ya mtoto wake?

Uliwashauri wanawake wajawazito bila kuwakandamiza wala kuwavunja moyo?

Ulimuacha mwanamke huyo mjamzito kufanya uamuzi?

Ulihakikisha kuwa uamuzi wa wanawake wajawazito unatokana na kuelewa vyema?

Uliorodhesha sababu zozote za kiafya, kijamii, kitamaduni na kidini kwa kufanya uamuzi tofauti – labda tofauti na ambayo ungependa kutimiza?

ElezaJe:

Ulitoa alichohitaji mteja huyo ikiwa hakuna sababu ya kiafya ya kutofanya hivyo?

Ulieleza wakati mwanamke huyo anafaa kukutembelea mojawapo ya dalili za hatari ikitokea?

Ulimsaidia kueleza kwa maneno yake jinsi anavyoelewa kila dalili ya hatari katika ujauzito?

Ulieleza kwa kutumia maagizo yaliyochapishwa, picha na michoro?

KurudiJe:

Mlipanga wakati wa safari itakayofuata?

Ulijadili na mwanamke huyo mjamzito kuwa anaweza kurudi na mumewe au mwenziwe?

Ulimhakikishia mwanamke huyo mjamzito kuwa anapaswa kurudi wakati wowote, kwa sababu yoyote?

Ulimhakikishia arudi karibuni hata ikiwa alikosa kuja siku aliyoratibiwa kwa sababu asizoweza kuepuka?

Ulimhakikishia kuwa ni haki yake kamili kwenda katika kituo chochote kingine cha afya wakati wowote?

Ulimshukuru mwanamke huyo mjamzito kwa kutembelea huduma ya utunzaji katika ujauzito?

15.5 Umuhimu wa kumhusisha mume/mwenzi katika ushauri wa ujauzitoni

Muhtasari wa Kipindi cha 15