Muhtasari wa Kipindi cha 15

Katika Kipindi cha 15 umesoma kuwa:

  1. Utoaji wa ushauri ni mchakato wa siri wa njia mbili za mawasiliano kati ya watu wawili unaowasaidia wanawake wajawazito kuchunguza maswala yao ya kibinafsi, kufanya uamuzi na kupanga jinsi ya kuchukua hatua ikiwa watapata dalili za hatari.
  2. Ujuzi wa kimsingi katika utoaji wa ushauri ni kusikiza kwa makini, kumhimiza mwanamke mjamzito kuongea, kuuliza maswali kwa uwazi na kumakinikia maswala husika yanayohusiana na dalili za hatari na umri wa ujauzito.
  3. Kila mwanamke mjamzito ana haki ya kuamua kitakachotendeka kwa ujauzito wake.
  4. Habari yote ambayo mwanamke mjamzito atatoa wakati wa majadiliao inafaa kuwekwa siri.
  5. Makosa ya kawaida katika utoaji wa ushauri ni kumkatiza mwanamke anapozungumza, kutazama kando mara kwa mara, kukosoa vikali maadili ya tamaduni na dini yake, kummalizia sentensi na kumhukumu.
  6. Mchakato wa utoaji ushauri hupitia awamu hizi: kufungua na kujenga uhusiano, kuchunguza maswala, kufanikisha mabadiliko, na kufunga.
  7. Mwanamke mjamzito anafaa kushauriwa kuja kwako mara moja ikiwa atapata mojawapo ya dalili hizi:
    • Kwa kawaida nusu ya kwanza ya muda wa ujauzito: kutapika mfululizo, kupoteza uzani, kutokwa na damu ukeni, na kukosa mabadiliko katika ukuaji wa fumbatio.
    • Kwa kawaida katika nusu ya pili ya muda wa ujauzito: maumivu ya kichwa, kiwaa, hisia ya kuungua kwa epigastriamu, kutokwa na damu ukeni, kuvuja kiowevu ukeni kukosa mabadiliko katika ukuaji wa fumbatio kupungua au kukosa kusonga kwa fetasi.
    • Wakati wowote katika ujauzito: joto jingi, kutapika, uchungu kwenye mwanya wa fupanyonga, macho kuwa manjano au kukohoa kulikodumu.
  8. Kumhusisha mume au mwenzi katika safari za utunzaji katika ujauzito huufanya utunzaji wa mwanamke mjamzito kuwa swala na jukumu la familia na pia huwasaidia kuwa macho kwa dalili za hatari zinazohitaji hatua ya haraka.

15.6 Orodha ya kukagulia baada ya kila kipindi cha ushauri katika ujauzito

Maswali ya kujitathmini ya Kipindi cha 15