17.3 Vipengele vya hatari ya KTW

Kupasuka kwa tando za fetasi unaweza kutokea wakati seviksi imefungwa au imepanuka. Wakati mwingine inaweza kutokea katika ujauzito wa mapema (baada ya wiki 28 - hii husababisha utokaji wa mimba usioweza kuepukika, ambayo utajifunza katika Kipindi cha 20), au katika awamu ya tatu (kati ya wiki 28 na wiki 34). Haijulikani nini husababisha kupasuka kwa tando za fetasi kabla ya kuanza kwa leba. Hata hivyo, kunavyo vipengele vya hatari vinavyohusishwa sana na KTW.

Zingatia kaviti ya amniotiki kuwa kifuko (au mfuko) ambacho kuta zake zimetengenezwa na tando za fetasi, zinazofungia fetasi na kiowevu cha amniotiki. Sehemu iliyodhaifu ya mfuko hupasuka, ambapo ni sehemu ya tando ambazo zimeshikana moja kwa moja na ‘mdomo’ wa seviksi. Upasukaji hutokea wakati mfuko umeharibiwa na maambukizi au jeraha la nje, au kupanuka zaidi (kuvimba) na kushindwa kustahimili shinikizo. Vipengele hivi vya hatari vimemeelezwa kwa ukamilifu hapo chini.

17.2 Uainishaji wa Kupasuka kwa Tando kabla ya Wakati (KTW)

17.3.1 Maambukizi yanaweza kusababisha KTW