17.3.5 Jeraha la fumbatio

Jeraha lolote butu au linalopenya kwa kuta za fumbatio linaweza kusababisha kupasuka kwa tando za fetasi. Majeraha butu hutokana na: daktari au mkunga kugusa uterasi ili kubadili mlalo wa fetasi kutoka hali ya miguu kutangulia au mlalo unaomkinga mama ili alale kwa hali kawaida ‘kichwa chini’ au kulala kwa veteksi; ukandaji wa uterasi na daktari wa kiasili; na majerahi butu ya fumbatio (kwa mfano, kutokana na pigo au kuanguka). Mfano wa jeraha la fumbatio linalopenya ni kuingiza sindano tupu kwa kaviti ya amniotiki kupitia kuta za fumbatio, au kupitia seviksi, ili kutoa kiowevu cha amniotiki au tishu ya plasenta ili kuifanyia uchunguzi.

17.3.4 Seviksi dhaifu

17.4 Utambuzi wa KTW