Malengo ya Somo la Kipindi cha 18

Ukimaliza kipindi hiki, unapaswa kuwa na uwezo wa:

18.1 Kufafanua na kutumia kwa ufasaha maneno yote muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito. (Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 18.1 na 18.2)

18.2 Kueleza hatari kwa mama, fetasi na mtoto mchanga za malaria, anemia na maambukizi kwenye njia ya mkojo wakati wa ujauzito. (Swali la Kujitathmini 18.1)

18.3 Kuwashauri wajawazito na waume zao jinsi ya kuzuia malaria, anemia, na maambukizi kwenye njia ya mkojo. (Swali la Kujitathmini 18.2)

18.4 Kutambua ishara na dalili za malaria kwa mjamzito, na kujua jinsi ya kudhibiti na wakati wa kumpa mama rufaa kwa kituo cha afya. (Swali la Kujitathmini 18.2)

18.5 Kutambua dalili za anemia kwa mjamzito, na kujua jinsi ya kudhibiti na wakati wa kumpa mama rufaa kwenye kituo cha afya. (Swali la Kujitathmini 18.2)

18.6 Kubainisha na kutofautisha kati ya ishara na dalili za maambukizi kwenye njia ya mkojo na ya figo wakati wa ujauzito, kudhibiti maambukizi yasiyokali kwenye njia ya mkojo wakati wa ujauzito na dawa za kumeza na kutambua wakati wa kumpa mama aliye na maambukizi yanayoendelea rufaa kwenye kituo cha afya. (Swali la Kujitathmini 18.2)

Mchoro 18.1 Baadhi ya aina ya mbu wanaoweza kusambaza parasiti za malaria kwa watu.

Kipindi cha 18 Matatizo ya Kiafya ya Kawaida wakati wa Ujauzito

18.1 Malaria wakati wa ujauzito