18.1.1 Dalili za malaria

Dalili za ugonjwa huwa ishara kwa mwathiriwa na anazifahamu na kuwa na uwezo wa kukueleza kuzihusu; wanaweza kukuambia pekee yao, lakini unaweza kuuliza maswali yanayozihusu. Dalili za malaria ni kama vile:

  • Baridi (kuhisi baridi isiyo ya kawaida) na kutetemeka (vipindi vikali vya kutetemeka kwa dakika kadhaa na hudumu hadi saa 1), hii huwa dalili ya kwanza ya maambukizi
  • Maumivu ya kichwa na udhaifu mara nyingi huandamana na baridi
  • Joto jingi mwilini (halijoto ya juu); Joto jingi mwilini mara nyingi hufuatwa na baridi, na joto linaweza kwenda juu sana hivyo mtu anakabiliwa na deliriumu (kutokuwa katika hali sawa kiakili, kuona au kusikia mambo yasiyohalisi)
  • Kutokwa na jasho joto lishukapo
  • Katika baadhi ya hali zingine kuhara/kutapika kunaweza pia kushuhudiwa
  • Dalili nyingine ya kawaida ni maumivu ya misuli/viungo.

Vipindi vya joto jingi kwa kawaida hubadilishana na vile vya baridi na joto kwa malengo ambayo yanaweza kuwa kila siku, au baada ya siku 2-3. Dalili hizi zote zinaweza kutokana na kitu kingine chochote, lakini unapaswa kushuku malaria ikiwa yatatokea kwa mtu ambaye ameumwa na mbu katika eneo ambalo malaria hutokea kila mara.

Mchoro 18.2 Mtu aliye na joto jingi mwilini atahisi joto zaidi kukuliko.

Ishara za ugonjwa ni ishara kuwa mhudumu wa afya pekee ndiye atakaye jua, au kutambua kwa kufanya uchunguzi. Kwa mfano, ukishuku ni malaria, unapaswa kupima halijoto na kipimajoto ukiwa nacho (ulijifunza jinsi ya kutekeleza haya katika Kipindi cha 9 ), au kwa kulinganisha hali yako ya joto na ya mama (Mchoro 18.2). Mtu akiwa na malaria, joto mwili linaweza kwenda juu hadi sentigredi 39-40 au hata zaidi.

  • Ni ipi kiwango cha joto la mwili la kawaida na ishara ya joto jingi mwilini ni ipi?

  • Joto la mwili kwa kawaida ni sentigredi 37; ishara ya joto mwilini litakuwa sentigredi 38 au zaidi.

    Mwisho wa jibu

18.1 Malaria wakati wa ujauzito

18.1.2 Utambuzi wa malaria