18.1.3 Matibabu ya malaria wakati wa ujauzito

Ni muhimu kwa wajawazito kuepukana na malaria - au kutibiwa haraka wakiwa wagonjwa. Dawa za kutibu malaria zinaweza kuwa na madhara, lakini ni afadhali kuliko kupatwa na malaria. Ikiwa mama ana dalili za malaria, anapaswa kutibiwa mara moja. Dawa inayotumika mara nyingi huitwa Artemether Lumifantrine (Inauzwa kama Coartem). Uharibu ukuaji wa parasiti katika seli nyekundu za damu za mtu.

Coartem inaweza kutumika kutibu malaria katika awamu ya pili na ya tatu ya ujauzito. Awamu ya pili ni wiki 13-27 tangu wakati wa mwisho wa mama kupata hedhi ya kawaida, na awamu ya tatu ni kutoka wiki 28 hadi wakati wa kuzaa, karibu wiki 40. Malengo ya uchunguzi yakionyesha kuwepo kwa malaria, au ukishuku kuwepo kwa malaria sana kulingana na ishara na dalili, na mama akiwa katika awamu ya pili ama ya tatu, mtibu kama ilivyoainishwa katika Kisanduku 18.1.

Kisanduku 18.1 Kutibu kwa kutumia Coartem katika awamu ya pili au ya tatu ya ujauzito

  • Tembe 4 za Coartem mara mbili kwa siku (baada ya masaa 12) kwa siku 3 (jumla ya tembe 24). Mshauri ameze na chakula, maziwa, supu au uji wa shayiri. Anaweza kuzivunja na kuzichanganya kwa kijiko cha chakula kama hii itakuwa rahisi kwake kumeza dawa. Mchoro 18.3 inaonyesha jinsi ya kueleza kina mama idadi ya tembe za kumeza.
  • Unaweza pia kumpatia tembe za paracetamol (miligramu 500-1000) kila baada ya saa 4-6 ili kupunguza joto jingi mwilini.
  • Kupanguza mwili wake kwa kitambaa kilichoingizwa ndani ya maji baridi pia husaidia akiwa na joto jingi.
  • Mshauri mama anywe maji mengi ili awe na maji ya kutosha mwilini. Anapaswa kunywa angalau kikombe1kubwa cha maji kila saa.

Wajawazito wanaoshukiwa kuwa na malaria katika awamu ya kwanza ya ujauzito, wanaoweza kusafiri, wanapaswa kupelekwa kwenye kituo cha afya kilichoko karibu kwa matibabu maalum.

Mama akiwa katika awamu ya kwanza ya ujauzito (yaani, hadi wiki 12 tangu wakati wa Mwisho wa mama Kupata Hedhi yake ya Kawaida), lakini anaugua sana kusafiri hadi kituo cha afya, mpe matibabu yaliyo katika Kisanduku 18.2. Hatari kwa maisha yake na ya fetasi kutokana na malaria, ni kubwa kuliko hatari ya kutumia dawa mapema wakati wa ujauzito. Mtume kwenye kituo cha afya haraka punde tu hali yake inapomruhusu kusafiri. Kumbuka kwamba dawa aina ya Artesunate huwekwa kwa kapsuli yenye umbo maalum - iitwayo sapozitori - katika njia ya haja kubwa kwa kusukuma polepole kupitia mkundu wake.

Picha 18.3 Mhudumu wa Afya anaonyesha chati chenye tembe za Coartem katika makundi manne. (Picha: hisani ya AMREF)

Kisanduku 18.2 Sidano ya Artemether na ya Artesunate kupitishwa kwenye mkundu

Sindano ya Artemether hudungwa kwa misuli kabla ya rufaa hali kali za malaria inaposhukiwa. Kwa kipimo cha miligramu 3.2 ya Artemether kwa kila kilo ya uzani wa mama, katika dozi moja kwenye misuli ya mkono wake upande wa juu.

Artesunate hupitishwa kwenye mkundu katika sapozitori kwa dozi zifuatazo kabla ya kupewa rufaa.

Uzani wa mamaDozi    Idadi ya sapozitori
Kilo 30-39Miligramu 50   1
Zaidi ya kilo 40Milingramu 4004

Kumbuka kwamba wajawazito wanaweza kuwa na uzani wa zaidi ya kilo 40 baada ya awamu ya kwanza ya ujauzito.

Jumla ya vifo vinavyotokana na malaria na magonjwa ya malaria zimepungua katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na jitihada kubwa za kuzuia malaria na matibabu ya haraka inapotokea. Mpango huu ni muhimu sana kwa kupunguza malaria hata zaidi, ikiwa ni pamoja na utambuzi na matibabu ya mapema kwa wajawazito wanaokuja kwenu kwa huduma ya ujauzito.

18.1.2 Utambuzi wa malaria

18.1.4 Kukinga malaria