18.1.4 Kukinga malaria

Ili kukinga malaria, lazima ufanye lote uwezalo ili usiumwe na mbu. Unapaswa kushauri kila mtu katika jamii wajitokeze pamoja ili:

  • Kuondoa maji taka yanayoleta mbu; ondoa maji ya mvua kwenye choo; funika au ondoa makopo ya bati na sufuria zinazokusanya maji karibu na nyumba.
  • Usikae usiku katika maeneo yenye maji ambapo mbu huzalia.
  • Tumia vyandarua vilivyotiwa dawa ya kuua wadudu, kemikali inayoua mbu. Katika maeneo mengi, unaweza kusambaza vyandarua vilivyotiwa dawa ya kua wadudu (tazama Picha 18.4) kwa familia zinazozihitaji. Vyandarua hivi vinalinda watu ambao hulala ndani yao kutokana na mbu, na wao pia hupunguza hatari kwa wale wengine wanaolala katika chumba kimoja nao kwa sababu dawa hii hufukuza mbu wasiingie ndani ya nyumba.
Picha 18.4 Vyandarua vilivyotiwa dawa ya kuua wadudu hutoa kinga nzuri kutokana na mbu wanaosambaza malaria. (Picha: UNICEF / Indrias Getachew)

Kukinga malaria inapaswa kuwa wajibu wa mtu binafsi na jamii. Panga kufanya kampeni ya afya kwa lengo la kuhamasisha wana nchi namna ya kukinga malaria, kwa kutumia mbinu za kukuza afya ulizojifunza katika Kipindi cha 2 katika Moduli hii. Hakikisha kwamba wajawazito unao wahudumia wanajua kwamba, watoto wao ambao hawajazaliwa na walio chini ya miaka 5 wote wako katika hatari ya malaria.

18.1.3 Matibabu ya malaria wakati wa ujauzito

18.2 Anemia katika ujauzito