18.2 Anemia katika ujauzito

Kina mama walio na anemia huwa na nguvu kidogo ya kuzaa na kuna uwezekano wa kuvuja damu sana baadaye (kuvunja damu nyingi baada ya kuzaa), wawe wagonjwa, au hata kufa baada ya kuzaa. Tayari umejifunza mengi kuhusu utambuzi na uzuiaji wa anemia katika vipindi vya mafunzo ya hapo awali katika Moduli hii, hivyo katika kipindi hiki tutazingatia tiba yake na kuimarisha ulichojifunza.

  • Je, anemia ni nini na nini hutokea katika mwili wa mtu aliye na anemia?

  • Mtu akiwa na anemia, kwa kawaida inamaanisha kuwa hajala vyakula vyenye ayoni ya kutosha. Seli nyekundu za damu huhitaji ayoni kutengeneza hemoglobini, kiungo kinachosaidia seli nyekundu za damu kubeba oksijeni kutoka kwa hewa tunayopumua hadi sehemu zote za mwili. Mtu aliye na anemia hawezi kutengeneza seli nyekundu za damu za kutosha, hivyo mwili wao una upungufu wa oksijeni.

    Mwisho wa jibu

Kumbuka kwamba baadhi ya aina ya anemia husababishwa na ugonjwa sio ukosefu wa ayoni na baadhi hurithiwa kutoka kwa wazazi (maumbile). Inaweza pia kusababishwa na parasiti fulani, ikiwa ni pamoja na malaria na minyoo. Katika kipindi hiki, tunashughulikia anemia inayosababishwa na upungufu wa ayoni kwa chakula. Wajawazito wengi wana anemia, hasa wanawake walio maskini ambao hawawezi kula vyakula vyenye ayoni ya kutosha, kama unavyojua kutoka Kipindi cha 14.

18.1.4 Kukinga malaria

18.2.1 Utambuzi wa anemia