18.2.1 Utambuzi wa anemia

Chunguza anemia kwa wajawazito wote kila mara wanapotembelea kliniki, kwa kuuliza kuhusu dalili zake. Maswali muhimu ya kuuliza ni:

  • 'Je, unajihisi mdhaifu au kuwa mchovu kwa urahisi?'
  • 'Je, unashindwa kupumua (upungufu wa pumzi) unapofanya kazi za kinyumbani?'
  • 'Je, unapata kizunguzungu mara nyingi, na umewahi kuzirai (kukosa fahamu)?

Dalili hizi husababishwa na oksijeni ndogo katika damu ya kumpatia nguvu ya kufanya shughuli za kawaida. Mtu aliye na anemia hujihisi kuwa ana upungufu wa pumzi kwa sababu wanahitaji kupumua kwa haraka zaidi ili kupata oksijeni ya kutosha katika miili yao. Ikiwa ubongo hautapata oksijeni ya kutosha, atahisi kizunguzungu na kuweza kuzirai.

Ishara za anemia (kinachochunguzwa au kupimwa na mhudumu wa afya) ni:

  • Weupe: uweupe ndani ya kope la jicho, viganja vya mikono, kucha, na ufizi.
  • Kupumua kwa kasi (zaidi ya mara 40 kwa dakika; kawaida kiwango cha kupumua ni mara18-30 kwa dakika).
  • Mpigo wa haraka kwa mshipa (zaidi ya mipigo100 kwa dakika). Ulijifunza jinsi ya kupima kiwango cha mipigo kwa mshipa katika Kipindi cha 9 (Sehemu ya 9.4).

Kwa ziara ya kwanza wakati wa utunzaji katika ujauzito

Ukishuku kuwa mama ana anemia, mshawishi afanyiwe uchunguzi wa anemia ikiwa huduma hiyo inapatikana katika Kituo cha Afya kilicho karibu. Uchunguzi wa damu hupima kiasi cha hemoglobini (ayoni iliyoko katika damu) ili kutathmini ikiwa inatosha kubeba oksijeni inayohitajika kwa shughuli za kawaida na mahitaji ya mtoto ambaye hajazaliwa kwa ukuaji. Ikiwa uchunguzi wa damu haupatikani, tumia utathimni wako wa ishara na dalili maalumu (zilizotajwa hapo juu) kutambua anemia na kutoa matibabu kama ilivyoelezwa hapo chini.

Kwa ziara ya baadaye wakati wa utunzaji katika ujauzito

Ukiwa na wasiwasi kuwa mjamzito ana anemia na haonyeshi maendeleo yoyote, unapaswa kumpa rufaa kwenye Kituo cha Afya mara moja.

  • Chunguza weupe ndani ya kope la macho yake, mikononi, kucha, na ufizi.
  • Hesabu mipigo wa mshipa wake. Je, ni zaidi ya 100 kwa dakika?
  • Hesabu mipigo anazopumua katika dakika 1. Je, ni zaidi ya 40?

Anemia ni hatari sana kwa afya ya mama na mtoto, hasa mama anapokaribia kuzaa.

18.2 Anemia katika ujauzito

18.2.2 Ukingaji wa anemia katika ujauzito