18.2.2 Ukingaji wa anemia katika ujauzito

Kula lishe bora

Wajawazito wote lazima washauriwe wale vyakula vilivyo na viwango vya kutosha vya ayoni na folate (vitamini, ambayo pia huitwa folic acid). Tayari unafahamu ni kwa nini anahitaji ayoni. Folate pia husaidia kukinga anemia kwa wajawazito au wanaonyonyesha, na inaweza kukinga baadhi ya hitilafu za kimaumbile kwa mtoto.

  • Rejelea Kipindi cha 13. Taja baadhi ya vyakula ambavyo vina ayoni nyingi.

  • Unaweza kuwa umefikiria baadhi ya vyakula hivi: kuku, samaki, alizeti, malenge na boga mbegu; maharagwe, mbaazi na dengu; mboga zenye rangi ya kijani kibichi; viazi vikuu; boga ngumu; nyama nyekundu (hasa ini, figo na nyama zingine za ogani); bidhaa za nafaka nzima kama vile mkate wa hudhurungi; mikate iliyowekwa ayoni (iliyoongezwa); karanga na kiini cha yai.

    Mwisho wa jibu

  • Taja baadhi ya vyakula vilivyo na folate nyingi.

  • Samaki; alizeti, malenge, na boga, mbegu; maharagwe na mbaazi; mboga zenye rangi ya kijani kibichi; nyama nyekundu (hasa ini, figo, na nyama nyingine); mchele wa hudhurungi; ngano nzima; uyoga na mayai.

    Mwisho wa jibu

Tembe za ayoni na folate

Unapaswa kumpatia mjamzito tembe za ayoni na folate za kutosha ili ameze tembe moja kwa siku, au tembe moja iliyounganishwa, hadi ziara ya utunzaji katika ujauzito inayofuata. Hakikisha unawaongeza kina mama tembe kila mara wanapozuru hospitali. Kipimo cha kuzuia ni:

  • Ayoni: Meza miligramu 300-325 za ferrous sulphate mara moja kwa siku, ikiwezekana na mlo. Kawaida kipimo hiki hutolewa kwa tembe moja iliyo pia na folate, lakini wakati mwingine inaweza kupeanwa kama matone ya ayoni.
  • Folate: Meza mikrogramu 400 za folic acid mara moja kwa siku, kwa kawaida imeunganishwa na ayoni.

18.2.1 Utambuzi wa anemia

18.2.3 Matibabu ya anemia wakati wa ujauzito