18.2.3 Matibabu ya anemia wakati wa ujauzito

Mama akiwa na anemia kali (Uchunguzi unaonyesha ana hemoglobini iliyo chini ya gramu 8 kwa lita moja ya damu) katika miezi 9 ya ujauzito, anapaswa kuzaa mtoto wake katika hospitali.

Anemia ya kawaida inaweza kutibiwa kwa kula vyakula vyenye ayoni na folate nyingi, na pia vitamini C (kama vile matunda ya jamii ya machungwa na nyanya), na kwa kunywa tembe za ayoni na folate. Kipimo cha kutibu ni:

  • Ayoni: Meza miligramu 300-325 za ferrous sulphate mara mbili kwa siku (mara mbili ya kipimo kinachotumika kwa kuzuia anemia).
  • Folate: Meza mikrogramu 400 za folic acid mara moja kwa siku kwa kinywa (kipimo sawa na kile cha kuzuia).

Baada ya kuagiza tembe hizi na ushauri wa lishe, mjamzito anayeshukiwa kuwa na anemia anapaswa kuchunguzwa tena baada ya wiki 4. Ikiwa hakuna maendeleo yoyote, mpe rufaa kwa kituo cha afya. Anaweza kuwa na ugonjwa, au anahitaji tembe za kuongezwa ayoni.

Tembe za kuongeza ayoni lazima zitolewe kwa miezi 6 wakati wa ujauzito kina mama chini ya 40% katika jamii wakiwa anemia. Endelea kwa zaidi ya miezi 3 baada ya kuzaa ikiwa zaidi ya 40% ya kina mama wana anemia, na mteja wako ananyonyesha.

Madhara ya tembe za ayoni

Matumizi ya tembe za ayoni yanaweza kusababisha madhara-kama vile kichefuchefu kufungika kwa choo na kinyesi cheusi. Mwambie mama anaweza kuwa na madhara-haya, lakini ni muhimu aendelee kutumia tembe za ayoni. Akimeza tembe baada ya mlo inaweza kumsaidia kuzuia kichefuchefu na unywaji wa viowevu vingi na ulaji wa matunda na mboga nyingi husaidia kuzuia kufungika kwa choo. Mhakikishie mama kuwa rangi nyeusi ya kinyesi chake hakina madhara na itaisha akimaliza tembe za ayoni.

Mchoro 18.5 Dalili na ishara kuu za maambukizi ya njia ya mkojo. (Tayari umeona miundo hii yote katika Mchoro 3.1 katika Kipindi cha 3, isipokuwa figo na mishipa ya figo.)

18.2.2 Ukingaji wa anemia katika ujauzito

18.3 Maambukizi kwenye njia ya mkojo