18.3 Maambukizi kwenye njia ya mkojo

Njia ya mkojo (tazama Mchoro 18.5) inajumuisha figo, mishipa ya figo, kibofu cha mkojo na urethra (ufunguzi ambapo mkojo hutokea nje ya mwili). Zote zimeshikamana na hufanya kazi pamoja ili kuondoa uchafu kutoka kwenye damu. Kwanza figo husafisha damu na kugeuza uchafu kuwa mkojo. Halafu mkojo huteremka kwenye mishipa ya figo hadi kwenye kibofu cha mkojo. Mkojo una katika kibofu cha mkojo mpaka mtu akojoe (kutoa maji).

Maambukizi kwenye njia ya mkojo hutokea wakati vimelea vilio na madhara (bakteria) huingia katika urethra. Maambukizi yanaweza kuenea kwa urahisi kwa kibofu cha mkojo au figo. Mara nyingi madaktari huyaita maambukizi kwenye njia ya mkojo. Unapaswa kuchukulia kuwa maambukizi kwenye njia ya mkojo yanaweza kuhusisha ngazi zote za njia ya mkojo: urethra, kibofu cha mkojo na figo.

Mama anaweza kupata maambukizi kwenye njia ya mkojo wakati wa ujauzito kuliko nyakati zingine zote. Maambukizi kwenye njia ya mkojo - hasa yanayofika kwenye figo - yanaweza kuwa hatari sana na pia kusababisha kuanza kwa leba mapema isipotibiwa mara moja. Ndio maana ni muhimu kuchunguza ishara za maambukizi katika kila ziara ya huduma ya ujawazito.

Mchoro 18.6 Kujipanguza kutoka mbele kuelekea nyuma baada ya kukojoa au kwenda haja kubwa husaidia kuzuia maambukizi kwenye njia ya mkojo.

18.2.3 Matibabu ya anemia wakati wa ujauzito

18.3.1 Kuzuia maambukizi kwenye njia ya mkojo