18.3.1 Kuzuia maambukizi kwenye njia ya mkojo

Ili kuzuia maambukizi kwenye njia ya mkojo, wafunze kina mama jinsi ya kuweka vimelea kwa vinyesi vyao mbali na njia ya mkojo kwa kujipanguza kutoka mbele kuelekea nyuma baada ya kukojoa au kwenda haja kubwa (tazama Mchoro 18.6). Iwapo watajipanguza kutoka mkundu kuelekea njia ya mkojo, wanaweza kuweka vimelea katika sehemu za siri na vinaweza kuingia kwenye urethra. Wakumbushe kina mama na wenzi wao wanawe mikono na kuosha sehemu za siri kabla ya ngono. Kina mama wanapaswa pia kukojoa mara tu baada ya kufanya ngono. Kutumia kondomu pia husaidia kuzuia kuenea kwa maambukizi katika njia ya mkojo kutoka kwa mwanaume hadi kwa mwanamke.

Katika Sehemu ya 18.3.3 (hapa chini), utajifunza jinsi ya kuwapatia antibiotiki kina mama ambao huwa na maambukizi kwa kibofu cha mkojo ili kuzuia maambukizi wakati wa ujauzito.

18.3 Maambukizi kwenye njia ya mkojo

18.3.2 Utambuzi wa MNM