18.3.2 Utambuzi wa MNM

Mama aliye na njia ya mkojo yenye afya si kawaida kuripoti maumivu, kuwashwa au uchungu wakati wa kukojoa. Hata hivyo, wakati mwingine mama anaweza kuwa na maambukizi kwenye njia ya mkojo lakini akakosa kuwa na dalili. Ni muhimu kujaribu kutambua ikiwa maambukizi yamefikia kibofu cha mkojo au ikiwa yamekwenda zaidi katika njia ya mkojo na kufikia figo. Maambukizi ya figo ni makali zaidi na ni hatari kubwa kwa mama na mtoto ambaye hajazaliwa.

Kuchunguza MNM

Maambukizi kwenye njia ya mkojo yanaweza kutambuliwa kwa kuchunguza mkojo wa mama. Kuna uchunguzi tofauti ambazo kawaida hutekelezwa katika Kituo cha Afya. Kuna kijiti cha kutumbukiza ambacho hubadilisha rangi inapoingizwa katika mkojo iliyoambukizwa au bakteria zinaweza kuonekana kama mkojo unachunguzwa kwa hadubini au bakteria zinaweza kukuzwa (kukuzwa) katika vyombo maalum hadi zitambuliwe. Uchunguzi huu wote unahitaji sampuli ya mkojo safi 'wa katikati unapokojoa’.

  • Ulijifunza jinsi ya kukusanya sampuli ya mkojo wa katikati unapokojoa katika Kipindi cha 9. Unawezaje kumweleza mama jinsi ya kufanya hivyo?

  • Utamwambia aanze kukojoa, lakini baada ya kutoa mkojo wa kwanza achukue kwa chombo safi baadhi ya mkojo wa katikati anapokojoa.

    Mwisho wa jibu

Kuwashwa au uchungu unapokojoa inaweza pia kuwa ni ishara ya maambukizi ukeni au magonjwa ya zinaa. Ikiwa utampata mgonjwa na dalili hizi, mpe rufaa kwenye kituo cha afya kilicho karibu.

Kijiti cha kutumbukiza, hadubini na uchunguzi wa kukuza bakteria ndio njia sahihi ya kutambua maambukizi katika njia ya mkojo, lakini huwezi kutofautisha maambukizi ya kibofu cha mkojo na ya figo. Unaweza kufanya hivyo tu kwa kumuhoji mama kwa makini juu ya dalili zake.

Dalili za maambukizi ya kibofu cha mkojo

Uliza mjamzito ikiwa amekuwa na dalili zozote zifuatazo:

  • Kuhisi haja ya kukojoa, kukojoa kila mara
  • Maumivu au uchungu unapokojoa au pindi tu baadaye
  • Maumivu katika fumbatio la chini, nyuma na mbele ya pelvisi.

Ukishuku maambukizi ya figo, mpe mama rufaa mara moja kwenye kituo cha afya kilicho karibu.

Dalili za maambukizi ya figo

Mchoro 18.7 Maumivu ya upande wa mgongo yanaweza kuwa ya kawaida katika ujauzito, au kuwa ishara ya maambukizi ya figo.

Uliza mjamzito ikiwa anahisi yafuatayo:

  • Dalili zozote za maambukizi ya kibofu cha mkojo
  • Mkojo unalio kama mawingu au damu
  • Joto jingi mwilini, kuhisi joto sana na kutokwa na jasho
  • Kujihisi mgonjwa sana au mdhaifu
  • Maumivu ya upande wa mgongo (upande mmoja au pande zote mbili)
  • Kutapika mara kwa mara
  • Baridi, joto, au kutetemeka sana.

Dalili nyingine ni maumivu upande wa chini wa mgongo, wakati mwingine kwa upande (tazama Mchoro 18.7). Lakini kumbuka kwamba maumivu ya mgongo ni kawaida katika ujauzito na huenda yasiwe ishara ya maambukizi ya figo. Maumivu ya kawaida kwa mgongo katika ujauzito yanaweza kusaidiwa na kusugua au mazoezi. Maumivu yakitokana na maambukizi ya figo, kusugua au zoezi halitamaliza.

18.3.1 Kuzuia maambukizi kwenye njia ya mkojo

18.3.3 Kutibu maambukizi ya kibofu cha mkojo