18.3.3 Kutibu maambukizi ya kibofu cha mkojo

Mshawishi mama anywe kikombe 1 kikubwa cha kinywaji safi na cha afya angalau mara moja kila saa kabla hajalala. Vinywaji husaidia kuondoa maambukizi kutoka kwenye njia ya mkojo. Maji ya kawaida na yale ya matunda ni mazuri hasa kwa kunywa. Mshawishi ale matunda ambayo yana vitamini C nyingi, kama vile machungwa, mapera ('zeituni') na maembe.

Maambukizi yasipopona haraka au mama akiwa na dalili yoyote ya maambukizi ya figo, mpe rufaa kwenye kituo cha afya, ambapo uchunguzi unaweza kufanywa ili kuthibitisha maambukizi na kuanza matibabu yanayofaa na antibiotiki (dawa za kuua bakteria). Unavyochelewa kutibu maambukizi, ndivyo itakuwa vigumu kutibu. Ukipata mafunzo ya kutibu magonjwa ya kibofu cha mkojo yasiyo makali na antibiotiki, kipimo ni:

  • Amoxicillin: Miligramu 500 kwa kinywa mara tatu kwa siku kwa muda wa siku 5; antibiotiki hii inaweza kutolewa katika tembe za miligramu 250 au 500, hivyo uwe makini unapotoa kipimo cha tembe sahihi. Kamwe usitoe antibiotiki nyingine – ila Amoxicillin tu.

Kutumia antibiotiki kuzuia maambukizi ya mara kwa mara katika kibofu cha mkojo

Mama akiwa na maambukizi kwenye njia ya mkojo mara kwa mara hapo awali, unaweza kumpatia matibabu ya kinga pamoja na antibiotiki ili kuzuia maambukizi zaidi wakati wa ujauzito. Kipimo ni:

Amoxicillin: Miligramu 250 mara moja kupitia kinywa kila siku wakati wa kulala hadi mwisho wa ujauzito na kwa wiki 2 baada ya kuzaa.

Ikiwa matibabu ya antibiotikiyatashindwa kutibu dalili za maambukizi au mama akipata maambukizi mengine ya kibofu cha mkojo baadaye katika ujauzito, mpe rufaa kwenye Kituo cha Afya kwa uchunguzi. Anaweza kuhitaji matibabu na antibiotiki mbalimbali.

18.3.2 Utambuzi wa MNM

18.4 Hitimisho