Muhtasari wa Kipindi cha 18

Katika Kipindi cha 18, umejifunza kwamba:

  1. Malaria inasababishwa na parasiti ambayo huenezwa na mbu.
  2. Mjamzito aliye na maambukizi ya malaria ana uwezekano zaidi wa kuwa na anemia, kuharibika kwa mimba, kuzaa kabla ya wakati, mtoto mdogo, mtoto kufa kabla ya kuzaliwa), au afe yeye mwenyewe.
  3. Ni muhimu kwa wajawazito kuepukana na malaria - kwa mfano kwa kutumia vyandarua vilivyotiwa dawa ya kuua wadudu - na kutibiwa haraka akiugua.
  4. Dawa za kutibu malaria zinaweza kuwa na gharama kubwa na madhara lakini dawa hizi ni salama zaidi kuliko kupatwa na ugonjwa wa malaria hasa wakati wa ujauzito. Dawa ya kawaida ya kutibu malaria ni Coartem.
  5. Ayoni husaidia damu kubeba oksijeni kutoka kwa hewa tunayopumua hadi sehemu zote mwilini. Ayoni kidogo katika mlo wa mjamzito inamaanisha atakuwa na pumzi kwa sababu ana anemia.
  6. Kina mama walio na anemia wana nguvu kidogo ya kuzaa na wana hatari ya kuvunja damu sana, kuugua au hata kufariki baada ya kuzaa.
  7. Kula lishe iliyo na ayoni na folate na kutumia madini hayo muhimu kwa tembe kila siku wakati wa ujauzito inaweza kuzuia anemia na kutibu hali za anemia sizizo kali.
  8. Njia ya mkojo hujumuisha figo, mishipa ya figo, kibofu cha mkojo na urethra. maambukizi katika njia ya mkojo ni ya kawaida wakati wa ujauzito na yanaweza kuzuiliwa kwa usafi.
  9. Maambukizi ya kibofu cha mkojo na figo yanaweza kuwa hatari kwa mama na pia kusababisha leba kuanza mapema mno yasipotibiwa mara moja. Unywe vinywaji safi na bora mara nyingi ya kutosha kuondoa bakteria mwilini.
  10. Kuwasha au uchungu wakati wa kukojoa ni dalili ya kawaida ya maambukizi ya kibofu cha mkojo, maambukizi ya kibofu yasiyo makali yanayoweza kutibiwa kwa antibiotiki. Antibiotiki ya kawaida katika kituo cha ngazi ya chini za afya ni Amoxicillin.
  11. Maambukizi ya figo hasa ni hatari na mama lazima wapewe rufaa mara moja akiwa na mkojo unayofanana na mawingu au ukiwa na damu, joto jingi mwilini na maumivu katika upande wa chini wa mgongo.

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi 18