Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi 18

Kwa kuwa umekamilisha kipindi hiki, unaweza kutathmini ulivyofaulu kutimiza Malengo ya Somo kwa kujibu maswali haya. Andika majibu yako katika shajara yako ya somo na uyajadili na Mkufunzi wako katika Mkutano ujao wa Somo Saidizi. Unaweza kulinganisha majibu yako na matini kuhusu Maswali ya Kujitathmini mwishoni mwa Moduli hii.

Swali la Kujitathmini 18.1 (yanatathmini Malengo ya Somo 18.1, 18.2 na 18.3)

Ni taarifa zipi kati ya zifuatazo zisizokweli? Katika kila hali, eleza kile kilicho sahihi.

  • A.Hatari ya MNM inaweza kupunguzwa kwa kunawa mikono na kuosha sehemu za siri vizuri.
  • B.Mama anaweza kupata maambukizi ya urethra, kibofu cha mkojo, au ya figo wakati wa ujauzito kuliko nyakati zingine.
  • C.Ni muhimu kumpatia mama tembe za ayoni ili kukinga anemia katika ziara ya kwanza ya huduma ya ujauzito.
  • D.Kumshawishi mama aliye na MNM anywe glasi 1 ya viowevu kila saa kabla hajala husaidia kupunguza maambukizi ya kibofu cha mkojo.
  • E.Malaria katika ujauzito huhusishwa na ongezeko la hatari ya kutoka kwa mimba pekee yake na mtoto kufa kabla ya kuzaliwa.
  • F.Maziwa ina folate nyingi, hivyo ukinywa maziwa mengi wakati wa ujauzito inaweza kukinga anemia.

Answer

A ni sahihi. Hatari ya MNM inaweza kupunguzwa kwa kunawa mikono na kuosha sehemu za siri vizuri.

B ni sahihi. Mjamzito anaweza kupata maambukizi ya urethra, kibofu cha mkojo, au ya figo wakati wa ujauzito kuliko nyakati zingine.

C si sahihi. Tembe za ayoni zinapaswa kutolewa wakati wa kila huduma ya ujauzito ili kukinga anemia - si tu wa kwanza.

D ni sahihi. Kushawishi mama aliye na MNM anywe glasi 1 ya viowevu kila saa kabla hajalala husaidia kupunguza maambukizi kwenye kibofu cha mkojo.

E ni sahihi. Malaria katika ujauzito huhusishwa na ongezeko la hatari ya utokaji wa mimba bila hiari na kufa kwa mtoto kabla ya kuzaliwa.

F si sahihi. Maziwa ni nzuri kwa kina mama wajawazito kama sehemu ya lishe bora, lakini haina folate; kwa hivyo anatakiwa kula samaki wengi, maharagwe, mbaazi, mboga yenye rangi ya kijani kibichi, nyama nyekundu, mchele ya rangi ya hudhurungi, ngano nzima, uyoga, na mayai ili kuongeza folate katika mlo wake.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 18.2 (yanatathmini Malengo ya Somo 18.1, 18.4, 18.5 na 18.6)

Kamilisha visanduku vilivyotupu katika Jedwali 18.1.

Jedwali 18.1 la Swali la Kujitathmini 18.2.
Hali ya afyaIshara na dalili
Malaria
Anemia
Maambukizi ya kibofu cha mkojo
Maambukizi ya figo

Answer

Jedwali 18.1 Toleo lililokamilishwa linaonekana hapa chini.

Jedwali 18.1 Ishara na dalili za kawaida za ujauzito-zinazohusiana na matatizo ya afya
Hali ya afyaIshara na dalili
MalariaBaridi, kutetemeka, maumivu ya kichwa, udhaifu, joto jingi mwilini ikibadilishana na baridi, kutokwa na jasho joto inapopungua, wakati mwingine kuhara/kutapika, maumivu ya misuli/viungo. Uchunguzi wa damu unaonyesha kuwepo kwa parasiti ya malaria.
AnemiaWeupe, kupumua kwa haraka (ugumu wa kupumua), mpigo wa haraka wa mshipa (zaidi ya mipigo 100 kwa dakika), udhaifu, kizunguzungu, kuzirai mara kwa mara. Uchunguzi wa damu unaonyesha kuna upugufu wa hemoglobini.
Maambukizi ya kibofu cha mkojoHisia ya kukojoa kila mara, uchungu au maumivi wakati wa kukojoa, maumivu katika tumbo upande wa chini. Bakteria huonekana kwa uchunguzi wa mkojo.
Maambukizi ya figoKama ilivyo kwa maambukizi ya kibofu cha mkojo, pamoja na mkojo wa rangi ya mawingu au damu kwa mkojo, joto jingi mwilini, kujihisi mgonjwa sana au mdhaifu, maumivu kwa ubavu katika pande moja au zote mbili ambayo haihuondolewi kwa kusugua, kutapika mara kwa mara, baridi na kutetemeka sana.

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 18